· Januari, 2010

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Januari, 2010

Rais wa Malawi kutangaza rasmi penzi lake siku ya Valentine

  30 Januari 2010

Wamalawi wanatafakari taarifa kuwa mnamo tarehe 1 Mei, rais wa nchi Dkt. Bingu wa Mutharika anatarajiwa kumuoa waziri wa zamani wa utalii Callister Moyo. Harusi hiyo itatanguliwa na sherehe za kitamaduni za uchumba wakati wa siku ya wapendanao ya Valentino tarehe 14 Februari. Wanabloga wachache wamemtakia heri rais katika mapenzi mapya aliyoyapata baada ya kifo cha mkewe Ethel miaka mitatu iliyopita.

Naijeria: Uzoma Okere ashinda kesi dhidi ya jeshi

  30 Januari 2010

Nigerian curiosity anaandika kuhusu kesi ya Uzoma Okere huko Naijeria: “Uzoma Okere ni msichana wa Kinaijeria ambaye kipigo alichopata kutoka kwa maafisa wa jeshi kiliondokea kuwa video iliyosambazwa sana na kuamsha hasira za wengi.”

Eritrea: Utawala Ulio Madarakani Uondelewe Haraka

  30 Januari 2010

Kwa mujibu wa Mohammed Hagos, mradi wa demokrasi katika Eritrea unapaswa uanze kwa kuuondoa madarakani utawala uliopo sasa: “Kikwazo kinachowazuia watu wa Eritrea kujieleza ni utawala wa Issayas. Njia ya kuelekea demokrasia kwa hiyo inaanza na kuuondoa utawala wa Issayas haraka iwezekanavyo…”

Kenya: Kiswahili Kuwa Somo La Kuchagua

  22 Januari 2010

Bunmi anaandika kuhusu uamuzi wa kulifanya somo la Kiswahili kuwa la kuchagua nchini Kenya: “Somo hili halitakuwa tena na mtihani wa lazima katika mtihani wa taifa wa darasa la nane…”

Marekani: Dkt. Martin Luther King, Jr. Akumbukwa

  22 Januari 2010

Martin Luther King Jr. alizaliwa tarehe 15 Januari, 1929 na akawa mmoja wa wasemaji na watetezi wakuu wa Harakati za Haki za Kiraia huko Marekani. Nchini Marekani, anaenziwa kwa sikukuu ya taifa, inayoadhimishwa kila mwaka siku ya Jumatatu ya tatu ya mwezi Januari. Leo, wanablogu wengi nchini Marekani wanaadhimisha kumbukumbu yake kwa kuandika makala za kumuenzi, huku wakiungalisha urithi wake wa masuala ya haki za jamii na masuala ya leo, wakionyesha wazi kuwa miaka 42 baada ya kuuwawa kwa King, maneno yake bado yana maana.

Afrika: Matangazo ya “AdWords” Katika Afrika

  13 Januari 2010

Miquel anajadili matangazo ya Google AdWords katika Afrika: “Wakati ingelikuwa ni njia nzuri sana kwa wanablogu wa Kiafrika kupata pesa kidogo ili kulipia gharama za intaneti, Google haitoi chaguo la malipo kwa nchi yoyote ya Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara.”

Togo Yaondolewa Kwenye Mashindano ya Kombe la Afrika baada ya Shambulizi Baya

  13 Januari 2010

Timu ya Taifa ya Togo sasa imeondolewa rasmi kutoka kwenye mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kufuatia shambulizi lililoelekezwa kwa msafara wa timu hiyo Ijumaa iliyopita katika eneo la Kabinda lililo nchini Angola na ambalo liko kwenye ukanda wa mapigano baina ya vikosi vya serikali na vile vya waasi wanaotaka kujitenga. Huku kukiwa na shutuma nyingi kutoka kwenye serikali ya Angola na maafisa wanaosimamia soka barani Afrika, wanablogu wa Ki-Togo wanauliza maswali magumu kuhusu msiba huo.

Angola: Kombe La Mataifa ya Afrika Moja Kwa Moja Kwenye Mtandao

  12 Januari 2010

Pata habari za Kombe la Mataifa ya Afrika yanayofanyika nchini Angola moja kwa moja: “Kwa wale ambao wangependa kuangalia Kombe la Mataifa ya Afrika 2010 kwenye mtandao, kutakuwa na tovuti za michezo zinazotoa mtiririko wa mapambano ya mpira moja kwa moja mtandaoni, bure.”