Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Disemba, 2011
Dondoo za Video: Maandamano, Chaguzi, Utamaduni na GV
Baadhi ya habari za kuvutia za Global Voices na video za hivi karibuni kutoka Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, Mashariki na Ulaya Kati, Karibeani pamoja na Marekani ya Kusini, zimeletwa na Juliana Rincón Parra.
Global Voices: Changia Leo
2011 umekuwa mwaka usio wa kawaida katika maudhui ya mtandaoni. Global Voices imekuwepo pale wakati mapinduzi yalipotokea, wakati tawala za kidikteta zikianguka, na matokeo ya matumizi ya mtandao yaliposambaa katika miji na mitaa ya wachangiaji wetu wanaoripoti kutoka duniani kote.
Rwanda: Watumiaji wa Twita Wajadili Mpango wa Rais Kagame wa Kugombea Awamu ya Tatu
Wakati mjadala wa ikiwa katiba ya Rwanda ibadilishwe kuruhusu muhula wa tatu uanzidi kupamba moto, Rais wa Rwanda Paul Kagame asema raia wanao uhuru wa kusema kwamba wanamhitaji. Mwandishi wa Kiingereza Ian Birell alijibu kwenye twita akisema, “Hawako huru, na kwa kweli ndivyo ilivyo, kusema aondoke…
Zimbambwe: Hasira wakati Mzee Mugabe Anapowania Uchaguzi wa 2012
Chama cha ZANU –PF (Zimbabwe African National Union - Patriotic Front) kimempitisha Robert Mugabe kuwa mgombea wake kwa ajili ya uchaguzi wa rais unaotazamiwa kufanyika mwaka ujao. Kama uchaguzi utafanyika mwakani, Mugabe atakuwa na umri wa miaka 88 na atakuwa Mwafrika wa pili mzee zaidi kugombea katika uchaguzi wa rais. Kupitia Twita na Facebook wa-Zimbabwe wameonyesha hasira na kutokuamini kilichotokea.
Zambia: Magari Mapya ya Kifahari ya Mtoto wa Rais Yasababisha Minong’ono
Taarifa zilizotangazwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya Kiraia ya Committee of Citizens, Gregory Chifire, kwamba mtoto wa kiume wa rais wa Zambia, Mulenga Sata, hivi karibuni alijipatia magari mawili ya kifahari, zimevutia hisia mchanganyiko kutoka kwa wa-Zambia watumiao mtandao
Madagaska: Wajadili Uhalali wa Uwekezaji wa Kigeni wa Moja kwa Moja
Wakati Madagaska ikijaribu kutafuta suluhisho la matatizo ya muda mrefu ya kiasa, Wanablogu wa ki-Malagasi wanajadili thamani ya Uwekezaji unaofanywa Moja kwa Moja na raia wa Kigeni. Wa-Malagarasi wanaamini kwamba Madagaska, kama nchi nyingine za Kiafrika inao utajiri mkubwa wa rasili mali lakini tatizo likiwa ardhi yenyewe kupokonywa kwa sababu ya utawala mbovu na biashara zisizoangalia maslahi ya wananchi.
Zambia: Rais Sata Aituhumu Benki Kuu Kuchapisha Noti Bandia
Rais Michael Sata ameweka wazi kwamba Benki Kuu ya Zambia kwa maelekezo ya kilichokuwa chama cha Upinzani nchini humo MMD, ilichapisha “noti bandia” ambazo inasemekana ziko kwenye mzunguko wa fedha. Hata hivyo, Chama cha MMD kwa kupitia Waziri wake wa zamani wa Fedha Situmbeko Musokotwane, kimekana tuhuma hizo kikisema Benki Kuu inayo uhuru wa kuchapisha noti mpya za ziada bila kuwasiliana na Waziri wa Fedha ama Rais kwa sababu ina mamlaka kamili ya kufanya hivyo.
Afrika Kusini: Malema Ameng’oka, Nini Kinafuata?
Mwanasiasa na mtu ambaye husababisha utata zaidi ya wote nchini Afrika Kusini Julius Malema amesimamishwa uanachama wa chama cha ANC kwa miaka mitano. Malema anachukuliwa na mashabiki wake kama sauti ya dhati ya watu masikini wa Afrika Kusini hususani kwa wito wake kuhusu utaifishwaji wa migodi ya Afrika Kusini.