· Februari, 2010

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Februari, 2010

Nijeria: Baada ya miezi miwili bila uongozi, kaimu Rais mpya

  28 Februari 2010

Baada ya wiki za mivutano ya kisiasa, Baraza la Seneti lilimthibitisha Goodluck Jonathan kama kaimu Rais. Wengi kwenye ulimwengu wa blogu waliliona tukio hilo kama sababu ya kusherehekea… lakini wengine waliliona kama jambo la kutia hofu, wakieleza kwamba japokuwa kutwaa madaraka kwa Jonathan kunaweza kuwa ni ulazima wa kisiasa, kutwaa huko hakujaruhusiwa wazi na katiba ya Naijeria.

Ghana: Mkuu wa Mkoa, Kofi Opoku-Manu, Anapoteza Umaarufu?

  27 Februari 2010

Mkuu wa Mkoa wa Ashanti, Kofi Opoku-Manu, hivi karibuni alionja joto ya jiwe kutokana na matamshi aliyoyatoa kwenye hotuba yake kwa mashabiki wa chama tawala, Nationa Democratic Congress (NDC) tarehe 6 Januari. Kwa mujibu wa Ato-Kwemena Dadzie, Opoku-Manu “aliwasihi mashabiki wa chama kutumia ghasia kusuluhisha tofauti zao.”

Mapinduzi Nchini Niger: Wanablogu Wapumua Pumzi ya Ahueni

  23 Februari 2010

Alhamisi Februari 18 mapinduzi ya kijeshi yalifanyika nchini Niger ambayo kwayo Rais Mamadou Tandja alikamatwa baada ya mapambano ya bunduki katika mji mkuu, Niamey. Miezi michache iliyopita Tandja alibadilisha katiba kinyume cha sheria ili ajiruhusu kuongoza kwa muhula wa tatu katika kile ambacho kilionekana kama dhuluma ya halaiki kwenye kura maoni. Wanablogu wanatoa mitazamo yao juu ya maendeleo haya mapya.

Je, Ghana Ipo Tayari kwa Upigaji Kura wa Kwenye Mtandao?

  22 Februari 2010

Tukio la siku mbili lililoanza jana; linaratibiwa na Danquah Instite (DI), kituo cha kutafakari sera, utafiti na uchambuzi, kutengeneza jukwaa la kitaifa kwa washikadau kuongoza majadiliano kuhusu uwezekano wa uanzishwaji wa kuandikisha wapiga kura kwa njia za vipimo vya kibaiolojia na hatimaye mfumo wa upigaji kura kwa njia ya mtandao nchini Ghana.

Ghana: Mapendekezo ya Kuvutia Kwenye Mapitio ya Katiba

  17 Februari 2010

Mwaka 2008, wakati wa Uchaguzi wa rais, wagombea waliwaahidi Waghana kuwa wangeitazama tena katiba ya nchi hiyo. Jambo lililoifanya ahadi hii kuonekana kama ni ya kweli lilikuwa ni nia ya wagombea – pamoja na Rais John Atta Mills – ya kuwashirikisha Waghana katika mchakato huo wa kuitathmini katiba. Inaonekana kuwa rais ametimiza ahadi hiyo, na sasa mapendekezo mapya yanachochea mijadala ya kuvutia.

Misri: Sisi Ni Washindi

Timu ya kandanda ya Misri iliifunga Ghana katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, na ikapata ushindi wake kwa mara ya tatu mfululizo. Huu pia ni ushindi wa saba tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo kwenye miaka ya hamsini. Wanablogu wanaungana na wananchi wa nchi hiyo kusherehekea mafanikio hayo.