Habari Kuu kuhusu Rwanda
Habari kuhusu Rwanda
Lugha za Pili Zinazoongozwa Kuzungumzwa Zaidi Afrika
Don Osborne anajadili habari iliyowekwa kwenye tovuti ya Chuo Kikuu cha Olivet Nazarene ikionesha ramani ya “Lugha za pili kuzungumzwa zaidi duniani.” Anaeleza matatizo makuu kutokana na habari hiyo: Suala la kwanza ni kudhani kwamba “lugha inayozungumzwa zaidi kwenye nchi yoyote huwa wazi; mara nyingi, ni lugha ya taifa husika.”...
Kupambana na Utapiamlo Nchini Rwanda Kupitia Muziki
Wanamuziki maarufu wa Rwanda King James, Miss Jojo, Riderman, Tom Close, and Urban Boyz walijiunga na mapambano dhidi ya utapiamlo nchini Rwanda kupitia video ya muziki kwenye mtandao wa YouTube. Video hiyo pia inapatikana kwa maandishi ya Kiswahili .
Kwa nini Rwanda Inaituhumu Ufaransa Kusaidia Mauaji ya Kimbari ya 1994
Wakati Rwanda ikiwakumbuka waathirika wa mauaji ya kimbari yalitokea miaka 20 iliyopita, Rais Kagame anasema tena kuwa Ufaransa lazima “ikabiliane na ukweli mgumu” wa kukiri kushiriki kwenye mauaji hayo ya mwaka 1994 [fr]. Kama matokeo ya matamshi hayo, serikali ya Ufaransa imesusia matukio yote ya kukumbuka mauaji hayo na waziri...
Fuatilia SafariYaGariAfrika Mtandaoni
Kikundi cha watengenezaji na wabunifu wa teknolojia kutoka Ulaya ambao wanadadisi ukuaji wa vituo vya teknolojia barani Afrika wanaendelea na safari yao ya gari barani humu. Tazama blogu yao au Tumblr na ufuatilie mjadala kuhusu safari yao kwenye mtandao wa Twita.
Mabadiliko ya Mfumo wa Ustawi wa Jamii ya Kiafrika
Utekelezaji wa mifumo ya hifadhi ya jamii ya taifa bado uko katika hatua za mabadiliko katika nchi nyingi za Afrika. Mafanikio ya mifumo iliyopo yanajadiliwa na wataalamu wa hifadhi za jamii katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara.
Rwanda: Watumiaji wa Twita Wajadili Mpango wa Rais Kagame wa Kugombea Awamu ya Tatu
Wakati mjadala wa ikiwa katiba ya Rwanda ibadilishwe kuruhusu muhula wa tatu uanzidi kupamba moto, Rais wa Rwanda Paul Kagame asema raia wanao uhuru wa kusema kwamba wanamhitaji. Mwandishi wa Kiingereza Ian Birell alijibu kwenye twita akisema, “Hawako huru, na kwa kweli ndivyo ilivyo, kusema aondoke…
Rwanda: Wanaomuunga Mkono wa Paul Kagame Wabaini Nguvu ya Twitter, Facebook na Blogu
Waungaji mkono wa rais Paul Kagame wa Rwanda wameanza kutumia nguvu ya ushawishi ya Facebook, Twitter na blogu ili kumsaidia kushinda uchaguzi wa rais unaotarajiwa kufanyika tarehe 9 Agosti 2010.
Rwanda: Video za Wanaojitolea
Mfululizo wa video zilizopakiwa na mtumiaji kdarpa kwenye YouTube, zinaonyesha wafanyakazi wa kujitolea na watu waliokutana nao wakiwa safarini nchini Rwanda ambapo walifanya kazi na jamii za sehemu hiyo.
Mwanamuziki mmoja wa Afrika Mashariki awashinda wengine wote kwa umaarufu wa mtandaoni duniani
Si wengi wanamfahamu kama Mwanaisha Abdalla bali Nyota Ndogo, ni jina linalojulikana kwenye kila nyumba katika Afrika Mashariki. Amekuwa akikusanya mashabiki wa mtindo wake wa kipekee wa Afrika Mashariki kwa miaka zaidi ya 4 sasa. Blogu yake, katika upande mwingine, imekuwa ikiendeshwa kwa muda wa miaka 3. Hapana shaka kuwa blogu hiyo imechangia ongezeko la kambi ya mashabiki kwenye mtandao wa intaneti.
Rwanda: Miaka kumi na tano baada ya mauaji ya Kimbari
Hivi karibuni zilifanyika sherehe za kitaifa nchini Rwanda kuadhimisha kumbukumbu ya kutimiza miaka 15 tangu mauaji ya Kimbari. Mauaji hayo yaliangamiza maisha ya watu wapatao 800,000. Mnamo tarehe 7 Aprili, maadhimisho yalifanyika katika mji mkuu wa Kigali, na pia katika mji wa Nyanza, ambapo watu wapatao 5000 waliuawa kinyama. Katika Uwanja wa Mpira wa Kigali, maelfu ya mishumaa iliwashwa na kupangiliwa katika namna ambayo iliunda neno "Matumaini" katika lugha tatu.