Habari Kuu kuhusu Cote d'Ivoire
Habari kuhusu Cote d'Ivoire
Mtazamo wa Tamasha la Kwanza la WanaBlogu na Vilogu wa Barani Afrika Lililofanyika Huko Dakar, Senegal
Kwa siku mbili, wanablogu na wanavilogu maarufu barani Afrika, wakiambatana na wadau kadhaa wa teknolojia barani Afrika walikuwa na majadiliano ya namna ya kuboresha kazi zao
Mfalme wa Rumba lenye Mahadhi ya ki-Kongo Afariki Dunia. Tunamkumbuka kwa Hili
Tumempoteza Papa Wemba, mwanzilishi wa rumba lenye mahadhi ya Kikongo na "mfalme wa Sape". "Kwaheri na asante sana kwa msanii huyu," tunasema sisi wa Global Voices
Yafanyike Mashambulizi Mangapi Dhidi ya Watalii Ili Afrika Magharibi Iandae Mkakati wa Pamoja wa Kikanda?
"Hatari haipo mbali kama tunavyoweza kufikiri. . . . Na pia, mashambulizi yana nafasi ndogo sana kuhusu amani ya ndani au uhusiano kati ya makundi ya kidini."
Mwanamke wa Ivory Cost Aangushwa Kutoka Ghorofa ya Sita kwa Kudai Mishahara yake
Msichana mwenye asili ya Ivory Coast alipoteza maisha kutokana na kile kilichotaarifiwa kuwa alisukumwa na mwajiri wake na kuanguka kutoka ghorofa ya 6 ya jengo kwa kile kinachodhaniwa kuwa ni ugomvi baina yao kuhusiana na malipo ya mshahara wa msichana huyo.
Mitandao ya Kijamii Yasaidia Kuikoa Côte d'Ivoire Iliyokumbwa na Mafuriko
Abidjan na maeneo mengine ya Côte d'Ivoire yamekumbwa na mafuriko makubwa katika majuma kadhaa yaliyopita [fr]. Wakazi wa maeneo husika walijipanga kwenye mitandao ya kijamii ili kusaidia namna ya kuwaokoa wananchi waliokuwa wamekwama kwenye janga hilo. Kwenye mtandao wa twita na facebook, #CIVSOCIAL ilikuwa ni alama ishara iliyokuwa ikitumika kwa...
Sababu za Kuishangilia Kodivaa kwenye Kombe la Dunia
Kwenye tovuti ya LaMula.pe, Juan Carlos Urtecho anaeleza sababu zake za kuishangilia Kodivaa kwenye mpambano wa Kombe la Dunia kati ya nchi hiyo na Kolombia siku ya Alhamisi, Juni 19: Desde que les ganaron a Japón en su debut, los marfileños se han vuelto mis preferidos en este mundial. […]...
Niger Yapata Kituo Chake cha Kwanza cha Reli Baada ya Kusubiri kwa Miaka 80
Aprili 7, Niger ilizindua katika mji mkuu wa Niamey kituo chake cha kwanza cha treni kuwahi [fr]. Mamlaka tayari ilikuwa na makadirio ya ujenzi wa kituo cha treni miaka 80 iliyopita lakini mradi kamwe haukuanzishwa. Tukio hilo litaanzisha ujenzi wa reli kati ya Niger, Benin, Burkina Faso na Côte d'Ivoire....
Mradi Mkubwa wa Reli Kati ya Mji wa Niamey na Cotonou Kuanza
Mradi wa reli wa urefu wa kilometa 1,500 kati ya Niamey, mji mkuu wa Niger na Cotonou, mji mkuu wa Benin umepitishwa na mamlaka ya nchi hizo mbili na ujenzi utaanza Machi 2014 [fr]. Francois Ndiaye katika Niamey anaelezea kuhusu makubaliano ya fedha [fr] inayojumuisha wadau mbalimbali na itasimamiwa na kundi la uwekezaji...
Watu 60 Wauawa kwa Msongamano nchini Abidjan
Magogo ya miti yaliyokuwa yameanguka barabarani yanaonekana kusababisha msongamano mkubwa na ulioua watu 60 na kujeruhi wengine 49 wakati wa sherehe za kuukaribisha mwaka mpya mjini Abidjan, Côte d'Ivoire. Kutokana na ukweli kuwa eneo hilo halikuwa na mwanga wa kutosha inawezekana ndio sababu iliyochangia tukio hilo la msongamano ulisababisha mkanyagano...
Côte d'Ivoire: Wafanyakazi wa Afya Wagoma baada Miezi Minne Bila Mshahara
S.B anatoa maoni juu ya kuanza kwa mgomo usio na ukomo unaoratibiwa na wafanyakazi wa taasisi za afya mjini Abidjan. Katika mtandao wa Connection Ivorienne, anabainisha [fr] kwamba: Kufuatia mabadiliko ya utolewaji wa huduma za afya ambazo zilitolewa bure kabisa baada tu ya kumalizika kwa mgogoro wa baada ya uchaguzi,...