· Machi, 2010

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Machi, 2010

Uganda: Wanafunzi Wacharuka, Kampala Yawaka Moto

Jumanne, majanga mawili tofauti yaliikumba Kampala, mji mkuu wa Uganda: wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Makerere walifanya ghasia baada ya wanafunzi wenzao wawili kupigwa risasi. Na makaburi ya Kasubi, ambayo ni sehemu ya Urithi wa Dunia ya UNESCO na eneo la kaburi la mfalme wa moja ya makabila makubwa zaidi ya Uganda, liliteketea kwa moto.

21 Machi 2010

Afrika Kusini: Ubaguzi wa Julius Malema

Wakati tabia za Rais Jacob Zuma zimekuwa zikizua mijadala mikali na yenye uhai katika ulimwengu wa blogu wa Afrika Kusini, hivi sasa ni mwanasiasa mwenye utata ambaye pia ni rais wa Umoja wa Vijana wa ANC, Julius malema ambaye anatengeneza vichwa vya habari. Hivi karibuni, aliwaongoza wanafunzi katika kuimba wimbo wa zamani wa kupinga ubaguzi wa rangi unaoitwa Ua Kaburu.

17 Machi 2010

Naijeria: Ghasia Zalipuka Huko Jos Kwa Mara Nyingine

Huko Jos, machafuko yanaelekea kujitokeza katika mizunguko inayozidi kuwa midogo: machafuko mabaya yaliukumba mji huo mwaka 1994, 2001, 2008, na – hata miezi miwili iliyopita – mnamo mwezi Januari 2010. Mgogoro wa sasa unasemekana kuwa ulianza katika tukio la kisasi kilichotokana na uharibifu uliotokea mwezi Januari, na, kama ilivyokuwa kwenye machafuko yaliyopita, mapambano ya sasa huko Jos yamekuwa yakipiginwa katika misingi ya kidini.

10 Machi 2010