· Machi, 2010

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Machi, 2010

Ghana: tamasha la Twestival 2010 Mjini Accra: Shughuli Yenye Maana?

  24 Machi 2010

Kama uanahabari wa kijamii unabadilisha mtindo ya mawasiliano katika nchi za Magharibi, basi kwa hakika haujapungukiwa katika kufikia sehemu zinazovutia barani Afrika. . Kwa hiyo haishangazi kwamba MacJordan, wa Global Voices, anashirikiana na Rodney Quarcoo ili kulifikisha tukio hili la kuburudisha kwa watu wa Ghana.

Martinique: Uchaguzi, utata na kugomea uchaguzi

  23 Machi 2010

Jumapili ya tarehe 14 Machi, raia wote wa Ufaransa wakiwemo wale wa idara za ng’ambo za Ufaransa walitakiwa kupiga kura... Lakini michakato miwili ya uchaguzi katika kipindi cha miezi mitatu inaweza kuwachosha 55.55% ya wapiga kura wa Martinique ambo waliamua kubaki majumbani.

Mali: Vitambaa Vyasuka Nguzo za Uchumi na Utamaduni

  23 Machi 2010

Kwa kupitia video, tunaona na kujifunza kuhusu umuhimu wa utamaduni na ongezeko la kiuchumi ambalo utengenezaji vitambaa huwapa baadhi ya watu na mashirika nchini Mali. Vikundi vya wanawake, wasanii na watalii wote wananufaika na utamaduni huu wa kutia rangi vitambaa na upakaji rangi kwa kutumia matope.

Uganda: Wanafunzi Wacharuka, Kampala Yawaka Moto

  21 Machi 2010

Jumanne, majanga mawili tofauti yaliikumba Kampala, mji mkuu wa Uganda: wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Makerere walifanya ghasia baada ya wanafunzi wenzao wawili kupigwa risasi. Na makaburi ya Kasubi, ambayo ni sehemu ya Urithi wa Dunia ya UNESCO na eneo la kaburi la mfalme wa moja ya makabila makubwa zaidi ya Uganda, liliteketea kwa moto.

Afrika Kusini: Ubaguzi wa Julius Malema

  17 Machi 2010

Wakati tabia za Rais Jacob Zuma zimekuwa zikizua mijadala mikali na yenye uhai katika ulimwengu wa blogu wa Afrika Kusini, hivi sasa ni mwanasiasa mwenye utata ambaye pia ni rais wa Umoja wa Vijana wa ANC, Julius malema ambaye anatengeneza vichwa vya habari. Hivi karibuni, aliwaongoza wanafunzi katika kuimba wimbo wa zamani wa kupinga ubaguzi wa rangi unaoitwa Ua Kaburu.

Mwaka Mmoja Baada ya Mapinduzi, Viongozi wa Madagaska Wakabiliwa na Vikwazo

  16 Machi 2010

Machi 17, 2009 nchini Madagaska, vikwazo vinavyowalenga viongozi wa sasa wa Madagaska vinaandaliwa kwa kushindwa kwao kuheshima makubaliano ya Maputo ambayo hapo awali yalifikiwa na pande zote zinazohusika. Matokeo ya vikwazo hivyo ni pamoja na kuzuiwa kwa mali zinazozalisha fedha na pengine kukamatwa kwa wanaohusika endapo watasafiri nje ya nchi.

Sudani: Je, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Itafanya Kazi?

  13 Machi 2010

Jarida la The Financial Times liliripoti hivi karibuni kuwa mpango wa mamilioni ya dola wa Benki ya Dunia wa kusambaza kompyuta na upatikanaji wa Intaneti huko Juba, mji mkuu wa Sudani ya Kusini, umeshindwa. habari hizi zinazua swali: kelele zinazoambatana na teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) zina uhalali?

Naijeria: Ghasia Zalipuka Huko Jos Kwa Mara Nyingine

  10 Machi 2010

Huko Jos, machafuko yanaelekea kujitokeza katika mizunguko inayozidi kuwa midogo: machafuko mabaya yaliukumba mji huo mwaka 1994, 2001, 2008, na – hata miezi miwili iliyopita – mnamo mwezi Januari 2010. Mgogoro wa sasa unasemekana kuwa ulianza katika tukio la kisasi kilichotokana na uharibifu uliotokea mwezi Januari, na, kama ilivyokuwa kwenye machafuko yaliyopita, mapambano ya sasa huko Jos yamekuwa yakipiginwa katika misingi ya kidini.

Kenya: Mafuriko Makubwa Yapasua Kingo za Mto Ewaso Nyiro Huko Samburu

  7 Machi 2010

Alfajiri siku ya Alhamisi, tarehe 4 Machi 2010, mafuriko makubwa yaliikumba Samburu huko kaskazini mwa Kenya na kuharibu nyumba 6 za kulala watalii watalii, baadhi ya kambi za utafiti wa wanyama pori na kuwaacha maelfu wakiwa katika paa za nyumba na kwenye miti. Wimbi hili la maji ya mafuriko lilikuja...