· Juni, 2009

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Juni, 2009

Togo Yafuta Adhabu ya Kifo

  28 Juni 2009

Bunge la Taifa la Togo limepiga kura ya kukomesha adhabu ya kifo na kuifanya nchi hiyo kuwa mwanachama wa 15 wa Umoja wa Nchi za Afrika kuipiga marufuku adhabu hiyo.

Msumbiji: Shambulio Dhidi Ya Mgombea Urais

  13 Juni 2009

Wanablogu wa Msumbiji wanaandika kuhusu shambulio dhidi ya mwanasiasa Daviz Simango, kwenye mji wa kaskazini wa bandari ya Nacala. Pamoja na maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu, chama cha Simango pia kilitumia huduma ya Twita kuandika kuhusu shambulio hilo.

Uganda: Mradi wa Katine Wawafikisha Wanakijiji Kwenye Ulimwengu wa Blogu

  9 Juni 2009

Inakadiriwa kuwa matumizi na uenezi wa intaneti nchini Uganda ni kwa kiwango cha asilimia sita tu, idadi ambayo inazuia sehemu kubwa ya watu kujiunga na ulimwengu wa blogu nchini Uganda au kuweza kuwasiliana na ulimwengu wa blogu duniani. Mradi wa Katine unaoendeshwa na Guardian and Observer unafanya kazi kubadilisha hali hiyo katika kijiji kimoja.

Malawi: Wasikilize wanablogu wa uchaguzi Malawi

  8 Juni 2009

Wamalawi wanapiga kura katika uchaguzi wa Raisi na Bunge. Baadhi ya wanablogu walipatiwa mafunzo na PenPlus Bytes, Taasisi ya kimataifa ya Uandishi wa TEKNOHAMA kwa ushirikiano na New Media Insitute kwa lengo la kuangalia na kutoa maoni yao kuhusu uchaguzi huo kwa kutumia blogu, teknolojia ya twita na simu za viganjani. Hebu na tuziangalie blogu zao, ambazo zimehifadhiwa katika Potal ya chaguzi za Afrika. Poto hii hutoa taarifa za kutosha kuhusu chaguzi mbalimbali katika nchi za kiafrika.

Uganda: Mke wa Rais ateuliwa kwenye Baraza la Mawaziri

  8 Juni 2009

Mabadiliko ya hivi karibuni katika Baraza la Mawaziri limewafanya wanablogu wa Uganda kuanza kubashiri matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2011. Moja ya uteuzi aliofanya Rais Yoweri Museveni ni ule wa kumteua mke wake, Janet, kuwa Waziri wa Nchi wa Karamoja. Eneo hili liko kaskazini-mashariki mwa Uganda na kwa miongo mingi limegubikwa na migogoro na umaskini uliokithiri.