· Oktoba, 2010

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Oktoba, 2010

Tanzania: Majumuisho ya Habari za Uchaguzi Mkuu wa 2010

  30 Oktoba 2010

Mnamo tarehe 31 Oktoba 2010, Watanzania watashiriki katika uchaguzi wa Rais wa Muungano, Rais wa Zanzibar pamoja na Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Huu ni mjumuisho wa yale yaliyojiri katika blogu mbalimbali kuhusiana na uchaguzi huo.

Tanzania: Ulimwengu wa Blogu Wachambua Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2010

  27 Oktoba 2010

Ifikapo tarehe 31 Oktoba 2010, Watanzania zaidi ya milioni 19.6 watafanya uamuzi muhimu kuhusu hatma ya nchi yao. Watafanya hivyo kupitia uchaguzi mkuu wa nne chini ya mfumo wa vyama vingi. Wakati zimebaki siku chache kabla ya uchaguzi huo, ulimwengu wa blogu wa Tanzania nao unafuatilia kwa karibu yale yanayotokea katika kampeni za vyama mbalimbali.

Tanzania: Matumizi ya Vyombo vya Habari vya Kijamii kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2010 Nchini Tanzania

  9 Oktoba 2010

Tanzania inaelekea katika uchaguzi wake mkuu mnamo Oktoba 31 mwaka huu na hivi sasa kampeni za uchaguzi zinaelekea kileleni. Wakati kampeni zikipamba moto, wagombea wa nafasi ya urais, ubunge na udiwani wameanza kutumia zana mpya za mawasiliano ya jamii ili kuwasiliana na wapiga kura. Sanjari na mikutano ya kampeni, ambayo hulenga watu wengi zaidi, idadi ndogo ya wanasiasa wameanza kutumia zana za mawasiliano ya kijamii kama vile blogu, picha za video za mtandaoni, Facebook na Twitter ili kukuza mawasiliano na wapiga kura.