· Mei, 2011

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Mei, 2011

Uganda: Polisi Wawanyunyizia Waandamanaji Rangi ya Waridi

  18 Mei 2011

Polisi wa Uganda wameikabili kampeni inayoendelea kwa mwezi mmoja sasa ya Kutembea Kwenda Kazini kwa kuwanyunyuzia waandamanaji moshi wa machozi na risasi sa moto. Wakati wa maandamano siku ya Jumanne, walitumia mbinu mpya, ya kuwashambula waandamanaji waliokuwa wakijaribu kuandamana kuelekea viwanja vya katiba katikati ya jiji la Kampala kwa maji yaliyochanganywa na uji wa rangi ya waridi.

Senegal: Harakati za “Imetosha Sasa Basi”: Kwanza Kwenye Mtandao, Na Sasa Ikulu

  10 Mei 2011

Wakati vuguvugu la mapinduzi likiendelea Uarabuni, matukio kadhaa ya vijana wenye hasira yamezuka katika tovuti za Senegal. Tangu mwanzoni mwa mwezi wa tatu, uanaharakati huo umeachana na ulimwengu wa mtandao na kundi linalojiita “Y'en a marre” (Imetosha Sasa Basi) sasa limegeuka na kuwa alama ya vuguvugu la upinzani. Founded in January 2011, Y’en a marre arose from frustration built up during power cuts that brought Senegal to a standstill. The group hails from the Dakar suburbs and is led by several local rappers, including Fou Malad, Thiat (from the group Keur Gui) and Matador.

Uganda: Wananchi Wakasirishwa na Kukamatwa Kikatili kwa Kiongozi wa Upinzani

  2 Mei 2011

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Dk.Kiiza Besigye alikamatwa tena katika mji mkuu wa Kampala kutokana na kushiriki kwake katika Kampeni ya Kutembea Kwenda Kazini usiku mmoja baada ya kuachiwa huru kwa dhamana. Besigye alipewa dhamana kwa sharti kuwa asijihusishe na kampeni ambayo imeuweka utawala wa Uganda kwenye vichwa vya habari kwa majuma matatu sasa.

Msumbiji: Polisi Washambulia Waandamanaji

  2 Mei 2011

Siku ya tarehe 6 Aprili, maofisa wa tawi la Polisi wa jamhuri ya msumbiji (PRM) – Kikosi cha Askari Maalum wa Dharura (FIR) – walitumia nguvukusitisha maandamano ya wafanyakazi wa shirika binafsi la ulinzi Group Four Security (G4S). Kwenye Facebook, wanamtandao walionesha kuchukizwa kwao kutokana na vitendo hivyo vya kikatili na kuhoji wajibu wa polisi, sheria na haki za binadamu.