Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Mei, 2014
Rwanda: Mema, Mabaya na Matumaini
Ingawa Rwanda imepiga hatua kubwa katika kuponya majeraha ya mauaji ya kimbari ya 1994, makundi ya utetezi yanaripoti vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu.
Je, Madaraka ni Matamu Kiasi cha Watawala wa Afrika Kushindwa Kuyaachia?
Gershom Ndhlovu anaangalia sababu za kwa nini watawala wa Afrika hawataki kuachia madaraka: Kumekuwepo na tetesi, dondoo na hata uvumi kuhusu afya au basi udhaifu wa afya ya Rais wa Zambia Michael Chilufya Sata, aliye madarakani tangu Septemba 2011. Tetesi hizi zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii kiasi kwamba serikali...
Naibu Waziri Ajinyonga baada ya Kushindwa Uchaguzi Nchini Malawi
Blogu ya City Press inaandika kwamba kujinyonga kwa Godfrey Kamanya, Naibu Wairi wa Malawi, baada ya kushindwa kukitetea kiti chake cha ubunge kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Mei 20, 2014 : Matangazo rasmi ya uchaguzi huo uliofanyika Jumanne bado yanaendelea kutangazwa. Lakini matokeo ya awali ya uchaguzi huo yaliyotangazwa na kituo cha redio yalionyesha...
Uchaguzi wa Malawi 2014
Malawi inapiga kura kumchagua rais siku ya Jumanne Mei 20, 2014. Fuatilia taarifa za moja kwa moja kwenye mtandao wa Twita @Malawi2014 na @MEIC_2014.
Mapigano ya Wanakijiji Kugombea Ardhi Yasababisha Maafa Nchini Madagaska
Blogu ya L'Express Mada ilitoa taarifa kwamba kijiji kizima cha Andranondambo kilichoko Kusini mwa Madagascar kiliharibiwa [fr] kufuatia mapigano ya wanakijiji yaliyosababishwa na mzozo wa kumiliki ardhi. Vita vya wenyewe kwa wenyewe, ambayo ilidumu kwa siku tatu kati ya Mei 20-22, ilipoteza maisha ya wanakijiji wote. Akikumbuka tukio hilo, mmoja...
“Hatujaweka Mkazo vya Kutosha Kwenye Afya ya Vijana”
Ripoti ya hivi karibuni kutoka kwa Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu afya ya vijana duniani inabainisha kwamba: Sababu kubwa za vifo vya vijana duniani ni ajali za barabarani, VVU?UKIMWI, na kujiua. Duniani kote, wastani wa vijana milioni 1.3 walipoteza maisha yao mwaka 2012. Ripoti inaongeza vile vile kuwa :...
Mashindano ya Kublogu ya AFKInsider
AFKInsider imeandaa mashindano ya kublogu ambapo mwanablogu bora kila mwezi atahitajika kuandika hadithi ya kulipiwa kila wiki kwa AFKInsider mwezi ujao: Mashindano ya wanablogu ya AFKInsider inanuia kugundua ubunifu wa wanablogu wa Biashara Afrika ambao huandika na wana nia ya teknolojia, kilimo, ujasiriamali, mali isiyohamishika, burudani, siasa, madini na habari...
Ethiopia: #FreeZone9Bloggers Yavuma Kwenye Mtandao wa Tumblr
Global Voices Advocacy ilianzisha mtandao wa Tumblr mapema mwezi Mei kutafuta uungwaji mkono kwa wanablogu tisa na waandishi wa habari – ambao wanne kati yao ni wanachama wa Global Voices – ambao kwa sasa wako kizuizini nchini Ethiopia shauri ya kazi zao. Washirika kutoka duniani kote waliwasilisha picha, ujumbe wa...
Ousmane Sow : Mwafrika Mweusi wa Kwanza Kushiriki katika Taasisi ya Kifaransa ya Sanaa
Mchonga sanamu Msenegali, Ousmane Sow, alikaribishwa kwenye Académie des Beaux-Arts de Paris [Taasisi ya Sanaa ya Paris] tarehe 11, mwezi wa Disemba. Africa-top-talents.com inaripoti kwamba: Une belle consécration pour ce sculpteur sénégalais connu pour ses séries de sculptures monumentales consacrées aux ethnies africaines (noubas, peuls, masaï, Zoulou). « Mon élection a d’autant plus de valeur à mes yeux...
Kutana na Joshua Beckford Aliyehudhuria Chuo Kikuu cha Oxford Akiwa na Umri wa Miaka 6
Blogu ya Omg Ghana iliripoti kuhusu mafanikio bora ya kielimu ya Joshua Beckford: Katika umri wa miaka 8, wewe pengine ulikuwa unafanya mazoezi ya michezo au ulikuwa ukifanya maandalizi ya kujiunga na daraja la tatu. Naam, kutana na Joshua Beckford mwenye umri wa miaka 8. Huyu yuko juu ya wastani wa...