· Disemba, 2009

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Disemba, 2009

Msumbiji: Je, ni Lugha Ngapi Zinazungumzwa Nchini?

  30 Disemba 2009

Kuna lugha 20 zinazozungumzwa nchini Msumbiji, kwa mujibu wa tovuti ya serikali, zaidi ya lugha ya serikali ya Kireno. Carlos Serra [pt] anajiuliza kama kuna lugha nyingine zaidi, kwa mujibu wa wataalamu wa lugha mashuhuri:”Kuna mtu aliniambia kuwa zipo kati ya 20 na 26; mwingine akaniambia zipo 17 zilizoandikwa na...

Malawi: Wanablogu Wajadili Matetemeko ya Ardhi 30 Katika Wiki 3

  30 Disemba 2009

Katika kile ambacho baadhi ya wataalamu wa miamba wamekieleza kama matukio ya nadra, Wilaya ya Kaskazini ya Karinga nchini Malawi imeshuhudia jumla ya matetemeko ya ardhi 30 katika wiki tatu zilizopita ambayo yamesababisha vifo 5, zaidi ya watu 200 kujeruhiwa na zaidi ya watu 3,000 kupoteza makazi. Wanablogu wamekuwa wepesi kushirikiana maoni.

Rwanda: Video za Wanaojitolea

  29 Disemba 2009

Mfululizo wa video zilizopakiwa na mtumiaji kdarpa kwenye YouTube, zinaonyesha wafanyakazi wa kujitolea na watu waliokutana nao wakiwa safarini nchini Rwanda ambapo walifanya kazi na jamii za sehemu hiyo.

Uganda: Rais Kuzuia Muswada Unaopinga Ushoga

  29 Disemba 2009

Muswada Unaopinga Ushoga wa 2009 uliopendekezwa nchini Uganda bado unasubiri uamuzi wa mwisho utakaotolewa na bunge la nchi hiyo, lakini gazeti la Daily Monitor lilitaarifu Jumatano kuwa Rais Yoweri Museveni ameihakikishia Idara ya Mambo ya Nje ya Marekani nia yake ya kuukwamisha muswada huo

Podikasti: Mahojiano na Sudanese Drima

Sudanese Drima ni jina la bandia la mwandishi wa Kisudani wa Global Voices anayeishi nchini Malaysia. Katika mahojiano haya ya dakika kumi tunajadili jinsi uanahabari wa kijamii unavyoathiri Uislamu, mgogoro wa dafur, na masuala ya nafsi ya Uafrika-Uarabu katika Asia ya Kusini Mashariki.

Misitu ya Madagascar Inateketezwa kwa $460,000 kwa Siku

  23 Disemba 2009

Wakati mataifa ya dunia yanakutana huko Copenhagen kwa ajili ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi, Madagascar, ambayo imekwishapoteza 90% ya misitu yake ya asili, inakabiliwa na tishio la biashara ya magendo ya magogo, inayotishia kuharibu kile kilichobakia katika moja ya mifumo ya mazingira yenye viumbe na mimea mingi inayotofautiana.

Ethiopia: Meles Zenawi aisaliti Afrika

  23 Disemba 2009

Lucas Liganga aandika kuhusu usaliti wa Waziri Mkuu wa Ethiopia: “kwa bahati mbaya, Waziri Mkuu wa Ethiopia meles Zenawi ambaye ni msemaji wa Afrika kuhusu mabadiliko ya tabianchi amejiunga na Ufaransa na kubadili nakala ya Afrika, jambo ambalo limewastua wajumbe wa Afrika.”

Wapiga picha wa Kiafrika, waandishi na wasanii wapata sauti zao kwenye blogu

  20 Disemba 2009

Kadri Waafrika wengi wanavyozidi kugundua nguvu ya kublogu kama zana ya kutoa maoni kwa kiwango cha dunia nzima, tarakimu ya wanablogu imeongezeka na pia maudhui yanayopewa kipaumbele. Kwa tarakimu hiyo ya kukua kwa blogu, wasanii wengi wa Kiafrika wamejiunga, na ongezeko kubwa likionekana kwenye blogu za mashairi kama ilivyo kwa upigaji picha unaochipukia na blogu za sanaa za maonyesho. Tunazipitia baadhi.