· Juni, 2012

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Juni, 2012

Umuhimu wa Kongamano La Sauti za Dunia (Global Voices Summit) hapa Nairobi

  27 Juni 2012

Kuanzia tarehe mbili mwezi wa Julai hadi tarehe nne mwezi huo huo, familia ya Sauti za Dunia (Global Voices, GV) pamoja na washiriki wao wa kimataifa, raia wapendao vyombo vya habari na watazamaji watakusanyika pamoja katika hoteli ya Pride-Inn mjini Nairobi kwa kongamano la GV. Bila shaka tukio hili ni la kusisimua na ambalo limekuwa likitarajiwa na wengi kwa shauku kuu.

Sudani: Kuondoa kizuizi cha Mapinduzi ya Sudani

  26 Juni 2012

Tofauti na nchi nyingine katika eneo lake, Sudani mara nyingi huwa haipati nafasi katika vyombo vikuu vya habari, na hili lilikuwa wazi zaidi wakati wa maandamano yalifanyika Ijumaa na Jumamosi. Sababu ni kwamba serikali ya Sudani imevibana mno vyombo vya ndani vya habari na kuwazuia waandishi kuripoti habari zinazohusu masuala ya haki za binadamu na ufisadi.

Sudani: “Polisi Yakanusha Kutumia Risasi; Majeruhi wote ni Wakufikirika

  24 Juni 2012

Maafisa wa serikali ya sudani wanarudia ‘uongo’ uliozoeleka ambao watawala wa ki-Arabu wamekuwa wakitumia tangu kuanza kwa yale yanayoitwa Mapinduzi ya Uarabuni yaliyoanza mwezi Desemba 2010. Imekuwa kawaida kusikia kauli kama, ‘waandamanaji wamedhibitiwa wakati wakiwashambulia polisi, ambao nao walijihami kwa kushambulia' Watumiaji wa mtandao wanaonyesha picha tofauti wakati tetesi zinadai mtandao wa intaneti utakatwa kufuatia kuongezeka kwa maandamano.

Kenya: Kilimo cha Bustani Mijini Chashika Kasi

  23 Juni 2012

Nchini Kenya, wakazi wa mjijini wanajifunza mbinu mbalimbali za kulima mazao ya chakula kwa ajili ya matumizi binafzi na kwa ajili ya kuuza katika maeneo madogo. kwa watu wenye kipato kidogo au wasio na kipato, ukulima wa mijini unaweza kuwa ndiyo ufumbuzi wa kujihakikishia uwepo wa chakula. Video hizi zinaonyesha jinsi ambavyo chakula kinaweza kuzalishwa katika makasha na vifaa vingine vya kubebea kwa kutumia maeneo na rasilimali kidogo.

Mabadiliko ya Mfumo wa Ustawi wa Jamii ya Kiafrika

  17 Juni 2012

Utekelezaji wa mifumo ya hifadhi ya jamii ya taifa bado uko katika hatua za mabadiliko katika nchi nyingi za Afrika. Mafanikio ya mifumo iliyopo yanajadiliwa na wataalamu wa hifadhi za jamii katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara.

Ethiopia: Ardhi, Historia na Haki katika Eneo la Gambella

  12 Juni 2012

Wanaharakati wa masuala ya ardhi wanatumia hati ya malalamiko ya mtandao, mtandao wa facebook na twita kufanya kampeni dhidi ya unyang’anyi wa ardhi nchini Ethiopia. Inaarifiwa kwamba wanakijiji kwenye jimbo msikini zaidi nchini humo, Gambella, wanalazimishwa kuhamia kwenye vijiji vilivyobuniwa na serikali ili kuwapisha wanaoitwa 'wawekezaji' wakubwa.

Kenya: Wanaharakati wapigana vita dhidi ya ufisadi kwa intaneti

  7 Juni 2012

I Paid a Bribe ni njia mojawapo inayotumiwa na wanaharakati dhidi ya ufisadi nchini, kwa kutumia teknolojia mpya ili kuwawezesha kupata ripoti za utoaji wa hongo.' I paid a Bribe' imefuatia muundo wa ‘India Anti-Corruption Portal (IPAB)' na ni ushirkiano kati ya IPAB na Wamani Trust ya Kenya ili kuleta IPAB katika Afrika Mashariki na Kati.