Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Oktoba, 2013
Kampeni ya Mtandaoni ya Kudai Amani Nchini Msumbiji
Blogu ya Mozmaniacos [pt] imezindua kampeni ya mtandaoni ya kudai amani nchini Msumbiji, kufuatia tishio la kuhatarisha amani iliyodumu kwa miaka 20 . Kwa kutumia kiungo habari #MozQuerPaz (#MozWantsPeace), watumiaji wa Facebook, Twitter, na Instagram waanza kuchangia picha zao pamoja na maoni yao kuhusiana na kampeni hii.
Zambia: Ukurasa wa Facebook wa Mke wa Rais wa Zamani Waghushiwa kwa Utapeli wa Ufadhili wa Masomo
Yeye si mtu maarufu nchini Zambia waliowahi kukuta akaunti bandia zikifunguliwa kwa majina yao. Ukurasa bandia wa Facebook kwa jina makamu wa rais wa nchi hiyo ilifunguliwa hivi karibuni.
‘Mwanablogu Mzuri Lazima Awe na Sifa za Asili za Waandishi Wazuri wa Habari’
Dorothée Danedjo Fouba, mshindi wa tuzo ya “Blogu Bora ya Teknolojia Afrika, iliyotolewa Tuzo za Uandishi wa Kiraia za Telkom-Highway Africa 2013“, alizungumza na Dibussi Tande (@dibussi) kuhusu maendeleo yake katika tasnia hii, na sifa zinazohitajika ili kufanikiwa.
Fuatilia SafariYaGariAfrika Mtandaoni
Kikundi cha watengenezaji na wabunifu wa teknolojia kutoka Ulaya ambao wanadadisi ukuaji wa vituo vya teknolojia barani Afrika wanaendelea na safari yao ya gari barani humu. Tazama blogu yao au Tumblr na ufuatilie mjadala kuhusu safari yao kwenye mtandao wa Twita.
Mwenendo wa Mashitaka ya Wanasiasa wa Kenya Mjini Hague
Mashitaka ya Kenya Hague ni mradi wa Dawati la Afrika la Radio Netherlands Worldwide kwa ushirikiano na This is Africa (Hii ni Afrika): Namna gani ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya mwaka 2007 na 2008 ziliathiri maisha yako? Unataka kufahamu nini kuhusu haki ya kimataifa? Changia habari ulizonazo, mawazo...
Hong Kong: Pinga Biashara ya Pembe za Ndovu
Muungano wa watu binafsi na Asasi Zisizo za Serikali zinazoguswa na tatizo la ujangili wa tembo, Hong Kong kwa Tembo, uliandamana Oktoba 4, wakiitaka Hong Kong kuteketeza hifadhi yake ya tani 25 za pembe za ndovu.
Gambia Yajitoa Jumuiya ya Madola, Yaiita Jumuiya Hiyo ‘Ukoloni Mambo-Leo’
"Gambia haitakuwa mwanachama wa taasisi yoyote ya ukoloni mambo-leo," nchi hiyo ya Afrika Magharibi ilitangaza katika tamko lake la wiki hii.
#EauSecours: AlamaHabari ya Kufanyia Mzaha Tatizo la Maji Dakar, Senegal
Dakar, mji kuu wa Senegal, umekumbwa na uhaba wa maji kwa siku 15 zilizopita [fr]. Wa-Senegali katika mitandao ya kijamii wanazoea tatizo hili kwa kufanyiana utani na uvumilivu. AlamaHabari (Hashtag) #eausecours (#H2OUT) inatumika hivi sasa kwneye mtandao wa twita na Facebook kutaniana kuhusiana na ukosefu wa maji safi unaoendelea, kama ilivyoonekana...
Zana ya Mtandaoni ya Kuwapima Wagombea Urais Nchini Madagaska
Tovuti ya ki-Malagasi iitwayo Madatsara imetengeneza tovuti utakayotumika kama majukwaa ya kuwapima wagombea wote wa Urais [fr]. Majukwaa yote yametengwa katika mada tisa kuwasaidia wananchi kufanya maamuzi ya busara wakati wa uchaguzi. Uchaguzi wa Rais umepangwa kufanyika tarehe 25 Oktoba, 2013 :
Katika Jamhuri ya Afrika, ”Bado Tuna Matumaini ya Kuishi Pamoja kwa Amani”
Kama mapigano baina ya waasi wa Sékéla na jeshi la taifa la Jamhuri ya Afrika ya Kati vinaendelea, mvutano katika mji wa Bossangoa. Wenyeji wanahofia kwamba migogoro inaweza kumwagika katika mapigano ya wazi kati ya jumuiya ya kikristo na Waislamu. Baadhi bado kushikilia tumaini kwa upatanisho angalau, kama Iman wa msikiti wa mji wa...