· Agosti, 2012

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Agosti, 2012

Nigeria: Rais wa Seneti Atakiwa Kuwataja Wafadhili wa Boko Haram

  31 Agosti 2012

Makundi mawili ya vijana Kaskazini mwa Nigeria Jumatano yalimkosoa Rais wa Seneti, David Mark, kutokana na matamshi aliyotoa siku za karibuni akiwataka viongozi wa mikoa ya kaskazini kudhibiti shughuli za kundi linaloogopwa sana la Boko Haram, Connected Africa anaripoti.

Kocha wa Timu ya Taifa ya Zambia Atunukiwa Ukaazi wa Kudumu

  30 Agosti 2012

Zambia imewahi kuwa na makocha wengi wa kigeni wa timu ya Taifa ya soka, lakini ni Mfaransa Herve Renard, aliyeongoza timu hiyo hadi kushina Kombe la Washindi Barani Afrika mwaka 2012, aliyepata upendeleo wa pekee. Ili kutambua mafanikio yake haya, serikali imemtunuku ukaazi wa kudumu lakini uamuzi huo unaonekana kuwekewa chumvi ya kisiasa.

Mauritania: Wafanyakazi wa Migodini Wapinga ‘Aina Mpya ya Utumwa’

  23 Agosti 2012

Zaidi ya wafanyakazi 2,300 wako kwenye mgomo nchini Mauritania katika mji wa kaskazini wa Zouerat, jambo ambalo limesababisha kuzorota kwa maeneo mengine kumi ya Kampuni la Taifa la Madini na Viwanda, huku kazi zikiwa kwenye mvurugiko mkubwa. Madai yamejikita katika suala zima la maslahi bora ya wafanyakazi.

Afrika ya Kusini: Yasherehekea Medali ya Kwanza ya Dhahadu Baada ya Miaka 8

  5 Agosti 2012

Pongezi nyingi zimekuwa zikimimika kwa muogeleaji wa Afrika Kusini Cameron van der Burgh ambaye amechukua medali ya kwanza ya dhahabu baada ya nchi hiyo kupata matokeo mabaya katika mashindano ya Olimpiki ya mwaka 2008 yaliyofanyika jijini Beijing. Amekuwa mwanaume wa kwanza wa Afrika Kusini kushinda medali ya dhahabu katika mashindano ya uogeleaji ya Olympics.