Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Aprili, 2012
Senegali:Rais Wade Aandamwa Hata Baada ya Kukubali Kushindwa Uchaguzi
Wakati nchi nyingine zikionekana kushangilia "uungwana" wa Bbdoulaye Wade kukubali matokeo nchini Senegali, wanablogu wa nchi hiyo bado wamemkaba koo Wade kwa kuushambulia Urais wake wakikumbushana ghasia za kuelekea uchaguzi, kubinywa kwa uhuru wa habari na mifano mingi ya utawala mbovu.
Naijeria: Gumzo la Mtandaoni Kuhusu Shirika la Ndege la Dominion
Kwa nini basi kuingia tu kwa jina jipya katika kibiashara ya safari za anga kusababishe majadiliano makali namna hii? Imetokea kuwa shirika hili la ndege si “la kawaida”: linasemekana kumilikiwa na Mtumishi wa injili ya “mafanikio, ” Askofu David Oyedepo.
Uganda: Ndiyo Tunampinga Kony!
Kampeni kwenye mitandao ya kijamii inayokusudia kuongeza uungwaji mkono wa harakati za kumkamata kiongozi wa waasi wa ki-Ganda na mhalifu anayetafutwa kwa udi na uvumba Joseph Kony imechukua sura nyingine.
Mali: Kimya cha Wanablogu wa Nchini Humo
Wakati mtandao wa intaneti umetawaliwa na blogu, ujumbe wa twita na video kutoka nchi mbalimbali, watumiaji wa intaneti wenyeji wa Mali wangali kimya. Mji mkuu, Bamako, umeathirika kwa kukatika kwa umeme kwa kile kinachodaiwa kuwa kuadimika kwa mafuta. Katika mazingira kama haya, kipaumbele si kutuma ujumbe, bali kutafuta kutafuta taarifa kuhusu viongozi wapya wa sehemu ya Kaskazini ya Nchi hiyo.
Ghana: Matumizi ya Vyombo vya Habari vya Kiraia katika Uchaguzi wa Mwaka 2012
Wananchi wa Ghana wanajitayarisha kwa ajili ya uchaguzi wa rais na wabunge ambao utafanyika tarehe 7 Disemba 2012, Jumuiya ya wanablogu wa Ghana imezindua mradi wa uanahabari wa kijamii ambao una nia ya kufunza wanaharakati, vikundi vya kisiasa na wanafunzi kutumia zana za uanahabari wa kijamii kwa ajili ya kwa ajili ya kuafuatilia na kuripoti shughuli za uchaguzi.
Zambia: Rais Awakera Raia Waishio Nje
Rais wa Zambia, Michael Sata, amewakasirisha raia wa nchi hiyo wanaoishi ng'ambo baada ya kuwakejeli wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini Botswana na kufifisha matumaini yao ya kuanzishwa kwa uraia wa nchi mbili katika Katiba ya nchi ya hiyo.
Mali: Raia Washtushwa na Mapinduzi ya Kijeshi
Askari walioasi wametangaza kwamba wanatwaa madaraka nchini Mali, baada ya kuwa wameteka nyara kituo cha televisheni ya taifa pamoja na ikulu. Wanadai kwamba serikali ilishindwa kuvipa vikosi vya jeshi la nchi hiyo msaada ili kuwakabili vilivyo wapiganaji wa kabila la Tuareg waliokuwa wakiteka miji ya kaskazini mwa nchi hiyo.
Tanzania: Mwigizaji Nyota wa Filamu, Steven Kanumba, Afariki Dunia
Tanzania ilimuaga mmoja wa wasanii wake maarufu na nyota wa tasnia ya filamu, Steven Kanumba, kwa maziko yaliyogubikwa na majonzi mazito mnamo tarehe 11 Aprili 2012. Alifariki alfajiri ya Jumamosi, akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kile kilichodaiwa kuwa ugomvi wa kimapenzi na rafiki yake wa kike aitwaye Elizabeth Michael kwa jina maarufu “Lulu”.
Congo (DRC): Video zasaidia kumtia hatiani Thomas Lubanga kwa uhalifu wa kivita
Mnamo tarehe 14, Machi, mahakama ya kimataifa ya makosa ya kivita ilimtia hatiani Thomas Lubanga, kiongozi wa zamani wa waasi Kongo (DRC) Mashariki, kwa kosa la kuwatumia watoto katika vita. Jaji alisema picha za video zilizoonyesha mahojiano na askari hao watoto ziliziongeza uzito wa ushahidi ulioisaidia mahakama kutoa hukumu.