Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Januari, 2010
Msumbiji: Kifo Cha Mradi Mkubwa wa Mazao Nishati
Mwishoni mwa mwezi Disemba, Baraza la Mawaziri la Msumbiji lilitoa tamko muhimu. Kibali cha kutumia Hekta 30,000 za ardhi kwa kampuni ya mazao nishati (biofuels) Procana, kimebatilishwa. Shauri la Mradi wa Procana, ulipo kwenye eneo kubwa linalopakana na Mbuga ya Taifa ya Limpopo ambayo imetanda mpaka nje mpaka wa nchi, lilikuwa na utata pamoja na mvutano mkubwa tangu (shauri hilo) lilipoanza mwanzoni mwa mwaka 2007.
Kenya: Video ya Fundi Baiskeli na Vifaa vya Kienyeji
Katika blogu ya Afrigadget kuna video ya fundi baiskeli anayeonyesha na kuelezea jinsi ya kutumia zana alizozitengeneza nyumbani wakati anafanya kazi zake katika soko jijini Nairobi.
Ethiopia: Adhabu ya Kifo Ili Kuwatisha Waethiopia
Berhanu Nega, mmoja kati ya watu waliohukumiwa kifo na mahakama ya Ethiopia anasema hashangazwi na adhabu ya kifo.
Sudani: Je, Umoja Bado Ni Chaguo la Kimkakati
Akiandika kwa Kiarabu, mwanablogu wa Kisudani Ayman Hajj anajadili siasa za nchi yake na kwa nini watu wengi wa Sudani wanapoteza imani katika umoja.