· Oktoba, 2009

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Oktoba, 2009

Ghana: Siku ya Kublogu mwaka 2009

  23 Oktoba 2009

Kwenye siku ya Kublogu Kwa Vitendo Duniani, Waghana waliwahoji viongozi wa dunia, walichachafya karatasi za Benki ya Dunia, walitambulisha tovuti mpya na walijiuliza ni kwa nini kulikuwa na majadiliano machache sana yanayohusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa nchini – na pia walitambua kwamba kuna mambo fulani nchi kama Ghana zinayafanya vyema.

Namibia: Kampeni ya Kukomesha Chanjo za Lazima

  19 Oktoba 2009

Kampeni ya kukomesha Chanjo kwa kulazimishwa nchini Namibia imezinduliwa: “ umoja wa Asasi za kijamii umetoa wito kwa Wanamibia wote kujiunga na kampeni ya kulaani chanjo kwa wanawake waishio na VVU bila ya ridhaa yao.

  17 Oktoba 2009

Mradi Wa Uchaguzi Afrika (AEP) www.africanelections.org utakuwa unafuatilia uchaguzi mkuu wa wa 10 wa Botswana, unaofanyika Oktoba 16, 2009.

Big Brother Africa msimu wa IV: Mageuzi yameanza

  17 Oktoba 2009

Big Brother Africa 4: Mapinduzi ni mfululizo wa nne wa vipindi vya kituo cha televisheni vinavyoonyesha maisha halisi vya Big Brother Africa, vilivyoanza Septemba 6, 2009. Kipindi hicho kimeshaanza kuzua mijadala na maoni kwenye mtandao wa intaneti kutoka kwa wanablogu na wasomaji wao.

  12 Oktoba 2009

Ripoti ya MISNA (Shirika La Kimataifa la Habari La Wamisionari) iliyochapishwa tarehe 25 Septemba inaeleza kuwa maandamano makubwa ya upinzani yalifanyika mjini Labe, jiji la pili kwa ukubwa nchini Guinea, dhidi ya Mkuu wa Nchi Mwanajeshi, Kapteni Moussa Dadis Camara.

Gabon: Upinzani waendelea kupinga matokeo ya Uchaguzi

  12 Oktoba 2009

Wapinzani wa kisiasa wa Gabon wanaonyesha muungano wa vyama vya siasa kupinga matokeo ya uchaguzi wa mwezi Agosti, ambayo yalimkabidhi urais mwana wa mtawala wa kiimla aliyepita, Omar Bongo. Wanasiasa na raia wanaikemea Ufaransa kwa kuingilia siasa za nchi hiyo.