Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Septemba, 2012
Mbinu za Kugundua Dawa Bandia katika Nchi Zinazoendelea
Watu 700,000 hufa kila mwaka kwa kutumia dawa bandia za malaria na saratani pekee. Shirika la Afya Duniani, WHO linasema katika ripoti yake kuwa, mapato kutoka kwa dawa hizi kila mwaka hukaribia dola bilioni 200.
Uganda: Binti awa Mbunge wa Kwanza Mdogo Kuliko wote Afrika
Afrika inachipuka na wanawake wa ki-Afrika wanachipuka nayo. Hivi sasa, Malawi na Liberia zinaongozwa na maraisi wanawake. Sasa nchini Uganda mbunge kinda kabisa kuliko wote barani Afrika amechaguliwa - naye ni Proscovia Alengot Oromait umri wa miaka 19 .
Je, Sifa ya ‘Kisiwa cha Amani’ Tanzania Imeanza Kutoweka?
Tanzania imeshuhudia matukio kadhaa mabaya tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa 2010. Tukio la hivi karibuni ni kifo cha kikatili cha mwandishi wa habari wa Tanzania Daudi Mwangosi, aliyeuawa kwa bomu la machozi huko Iringa, Kusini mwa Tanzania, wakati polisi walipojaribu kukitawanya kikundi cha wafuasi wa chama cha upinzani.
Kocha Mfaransa Ateuliwa Kuongeza Bahati ya Kenya Kwenye Kandanda
Shirikisho la Kandanda nchini Kenya FKF, limemchagua Kocha mpya wa timu ya taifa la Kenya ambaye ni Mfaransa, Henri Mchel. Wanakamati hao, wana matumaini kuwa anaweza kuwa 'bahati' ya Kenya katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya 2013 na Kombe la Dunia la 2014.
Afrika: Tuzo la Mbuyu wa Dhahabu
Wasilisha kisa chako upate fursa kushinda Tuzo ya Mbuyu wa Dhahabu: “Tuzo ya Mbuyu wa Dhahabu ilianzishwa mwaka 2008 kuwahamasisha waandishi wa ki-Afarika waliojikita katika vitabu vya watoto na vijana.”...
Paralympiki 2012: Mwanzo mzuri, Habari za Kukumbukwa
Martine Wright, aliyenusurika mlipuko wa mabomu uliotokea London, Rim Ju Song, mshiriki wa kwanza kutokea Korea Kaskazini ambaye, miezi michache iliyipita, hakuweza kuogolea; na Hassiem Achmat, ambaye alinusurika kuuawa na papa aliyemshambulia akiwa baharini. Baadhi tu ya washiriki wakuu wa mashindano ya Paralympiki. Martine Wright, aliyenusurika mlipuko wa mabomu uliotokea London, Rim Ju Song, mshiriki wa kwanza kutokea Korea Kaskazini ambaye, miezi michache iliyipita, hakuweza kuogolea; na Hassiem Achmat, ambaye alinusurika kuuawa na papa aliyemshambulia akiwa baharini. Baadhi tu ya washiriki wakuu wa mashindano ya Paralympiki.
Global Voices Yashinda Tuzo Ya Highway Africa
Timu ya Global Voices inayoandika habari za Nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara imeshinda Tuzo ya Telekom Highway Africa katika kundi la “Blogu bora ya TEHAMA ya...