· Oktoba, 2008

Habari kuhusu Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Oktoba, 2008

Afrika ya Kusini: VVU na UKIMWI na mabadiliko ya sera

  26 Oktoba 2008

Mwishoni mwa mwezi Septemba, Barbara Hogan, aliteuliwa na Rais wa mpito Kgalema Motlanthe kuwa waziri mpya wa afya wa Afrika ya Kusini, akichukua nafasi ya mtangulizi wake mwenye utata mwingi, Manto Tshabalala-Msimang. Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI na raia wengi wa Afrika ya Kusini wana matumaini makubwa kwamba hatua hii...

Madagascar: Kuishi ughaibuni hubadili uhusiano

  21 Oktoba 2008

Katika makala iliyochapishwa mwezi Machi, wachumi William Easterly na Yaw Nyarko wanaeleza kwamba katika nchi zilizo chini ya Jangwa la Sahara, kiasi cha fedha kinachotumwa na wahamiaji wanaotoka bara hilo ni wastani wa asilimia 81 ya misaada ya fedha kutoka nchi za kigeni kwa kila nchi. Dhima ya waMadagascar walio...

Macho ya Kimataifa kwenye Uchaguzi wa Marekani

  15 Oktoba 2008

Kadiri uchaguzi wa Marekani unavyokaribia, ndivyo kadiri macho ya kimataifa yanavyozidi kuelekezwa katika sera za nje za taifa hilo na wagombea wake wakuu. Kazimiradi kama vile ile ya Collective Journalism inayofanywa na Current TV (Uandishi wa Habari wa Umma wa Current TV) na Global Voices' Voices Without Votes (Mradi wa Global Voices - Sauti Zisizo na Kura) zimechukua jukumu la kukusanya taarifa na kuzipa mtazamo wa kimataifa katika masuala ya ndani ya sehemu fulani tu ulimwenguni.

Mwangwi wa Sakata la Maziwa China katika Afrika

  1 Oktoba 2008

Nchini China inakadiriwa kuwa watoto 13,000 wameugua tangu sakata la maziwa yasiyofaa kuibuka. Ushawishi na nguvu za China vimeongezeka Afrika, kama ulivyoongezeka uagizwaji wa bidhaa za kila namna, kuanzia viatu vya mazoezi mpaka chakula aina ya tambi. Mabloga hata wale walio mbali kama Kongo au Senegal, wanaguswa na usalama wa bidhaa za kutoka China katika nchi zao, na wanafuatilias habari hiyo (ya maziwa yasiyofaa).

Afrika Ya Kusini: Mjomba, Urais Uko Wapi?

  1 Oktoba 2008

Ulimwengu wa blogu nchini Afrika ya Kusini umelipuka kutokana habari za hivi karibuni kuhusu mawaziri 11 na manaibu 3 kujiuzulu wakiwemo mawaziri vinara, Trevor Manuel na Naibu Rais, Phumzile Mlambo-Ngcuka. Yafuatayo ni yale wanayosema mabloga …