· Machi, 2012

Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Machi, 2012

India: Gazeti pekee duniani linaloandikwa kwa mkono

  31 Machi 2012

Magazeti ya mwanzo yalikuwa yakiandikwa kwa mkono. Inawezekana kwamba hivi sasa gazeti la ‘The Musalman‘ pengine ndiyo pekee lililobaki linaloandikwa kwa mkono ulimwenguni. Gazeti hili linalochapishwa kwa lugha ya Ki-Urdu lilianzishwa mwaka 1927 na Chenab Syed Asmadullah Sahi ambapo hivi sasa linachapishwa kila siku katika jiji la Chennai huko India tangu kuanzishwa kwake.The earliest forms of newspaper were handwritten and now 'The Musalman' probably is the last handwritten newspaper in the world. This Urdu language newspaper was established in 1927 and has been published daily in the Chennai city of India ever since.

Dondoo za Video: Utetezi wa haki za binadamu

Kuna masimulizi kusisimua katika siku za hivi karibuni kwenye tovuti ya Global Voices Video za Utetezi ikiwa ni pamoja na haki za wananchi wenyeji na habari za hivi karibuni kutoka Amerika ya Kusini, Mashariki ya Mbali, Ulaya Magharibi na Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara zilizochaguliwa na Juliana Rincón Parra.

Iran: Wanawake wapinga ‘Jinamizi la Vita’

25 Machi 2012

Utawala wa Kiislamu wa Iran umepuuza Siku ya Wanawake Duniani kwa zaidi ya miongo mitatu. Utawala huo hauitambui siku ya Machi 8, na umepiga marufuku mashirika ya wanawake kusherehekea siku hiyo. Lakini kila mwaka wanawake wa ki-Iran iwe kwa uwazi ama kificho bado wanasherehekea siku yao hiyo.

Korea Kusini: Wahudumu wa ndege wapigania haki ya kuvaa suruali

  25 Machi 2012

Katika Siku ya Wanawake Duniani, wahudumu wa moja ya mashirika makubwa ya ndege nchini Korea Kusini, waliitisha mkutano na waandishi wa habari mbele ya makao makuu ya shirika lao la ndege kudai haki ya kuvaa suruali. Madai hayo yamepata uungwaji mkono mkubwa sana na watumiaji wa mtandao wa nchini humo.

Iran: Wachora katuni ‘wamkalia kooni’ Khatami kwa kupiga kura

24 Machi 2012

Mohammad Khatami, aliyekuwa Rais mwanamageuzi wa Irani, Ijumaa ya tarehe 2 Machi, 2012 alipiga kura katika uchaguzi wa wabunge. Kitendo hicho kilikinzana na kauli aliyopata kutoa siku za nyuma kwamba angegomea kupiga kura hadi wafungwa wote wa kisiasa waachiwe huru na katiba kuheshimiwa. Kitendo chake hicho kimezua shutuma nyingi kutoka kwa wanamageuzi walio makini katika kugomea uchaguzi huo.

Amerika Kusini: Waathirika wa ‘biashara’ ya kukuza matiti waingia mtandaoni

  24 Machi 2012

Wanawake wengi wameungana kwenye tovuti za kijamii kusema wanachofikiri na kubadilishana taarifa kuhusu matatizo yanayosababishwa na viini vya kukuzia matiti. Wakati huohuo wanapanga hatua gani za kisheria wachukue. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ugonjwa wa saratani huko Amerika ya Kusini. Je, ni kina nani hawa wanaopaaza sauti zao barani humo? Fuatilia ...