· Januari, 2012

Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Januari, 2012

Ivory Coast: Mjadala Mkali dhidi ya Chombo cha Habari kilichotumia Picha za Mwanablogu Bila Ruhusa

For the blogger and professional photographer Audrey Carlalie, the Christmas 2011 holidays were marked by the fact that her photos of a celebratory firework display were used by certain Ivorian newspapers without her authorization. Kanigui reports.For the blogger and professional photographer Audrey Carlalie, the Christmas 2011 holidays were marked by the fact that her photos of a celebratory firework display were used by certain Ivorian newspapers without her authorization. Kanigui reports.

Makala za Global Voices Zilizosomwa Zaidi mwaka 2011

Global Voices haijabaki kuwa sauti pweke ya vyombo vya habari vya kiraia linapokuja suala la twita zinazotuma taarifa na posti za kwenye blogu. Bado, hata hivyo pale ambapo shauku kwa vyombo vikuu vya habari ikindelea kupungua, sisi ndio tunaojibidiisha kuendelea kuweka kumbukumbu ya kile ambacho wanablogu wadogo popote pale waliko wanahitaji dunia ikifahamu. Fahamu orodha ya makala zetu 20 zilizosomwa zaidi kwa mwaka 2011

Venezuela: Ziara ya Mahmoud Ahmadinejad Yaibua Utata

  25 Januari 2012

Rais wa Iran, Mahmud Ahmadinejad, aliwasili nchini Venezuela Jumapili, Januari 8, katika kituo chake cha kwanza cha ziara ya ya nchi kadhaa za Marekani ya Kusini. Ziara yake imechochea miitiko mikali kweny mitandao ya kijamii, ambako watumiaji wanahoji kama uwepo wake unaweza kuwa na faida yoyote kwa taifa.

Venezuela: Mwanaharakati wa mtandaoni Luis Carlos Díaz anyanyaswa na kutishwa na “wezi wa akaunti za mtandaoni”

GV Utetezi  25 Januari 2012

Kwa mara ya pili ndani ya kipindi cha miezi minne tu, mwandishi wa habari wa Venezuela na mwanaharakati, Luis Luis Carlos Díaz, amenyanyaswa kupitia akaunti yake ya Twita [1] na simu yake ya mkononi na kikundi kinachojulikana kama cha "wezi wa akaunti za mtandaoni", na ambao hutumia jina la N33 [2], na bila shaka ni kundi lilelile la watu ambao miezi michache iliyopita liliiba maneno ya siri ya akaunti za Twita na baruapepe ya karibu watu thelathini maarufu wa Venezuela, baadhi yao ni waandishi wa habari Sebastiana Barráez, Ibéyise Pacheco, mchekeshaji wa kisiasa Laureano Márquez, mwanaharakati Rocío San Miguel na mwandishi Leonardo Padrón, miongoni mwa wengine wengi.

Singapore: Maoni ya Waziri Yasababisha Tafrani Mtandaoni

  16 Januari 2012

Fahamu kwa nini sentensi hii “Nilipofanya uamuzi…” imezua tafrani mtandaoni nchini Singapore inayotokana na kauli iliyotolewa na waziri mwandamizi wa nchi hiyo. Hiyo ni kufuatia uamuzi wa serikali kupunguza mishahara ya wanasiasa ambao ni kati ya watu wanaolipwa zaidi duniani.