· Januari, 2011

Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Januari, 2011

Kazakhstan: Wanablogu Wajadili Dini

  31 Januari 2011

Kwa kuwa Kazakhstan haina sera bayana ya dini, imekuwa ada kwamba kila mtu ana uhuru wa kuwa na mtazamo wake katika masuala ya kiimani. Kama ilivyokuwa miaka ishirini iliyopita, hakuna ambaye kwa hakika anajishughulisha na mitazamo hii lukuki ya kidini, ambayo inathibitishwa na mjadala kuhusu dini na desturi , ambayo...

Dunia ya Uarabu: “Acheni Kulia Juu Sudani”

  31 Januari 2011

Kura ya maoni kwa ajili ya uhuru wa Sudani ya Kusini leo imeiweka nchi hiyo kwenye uangalizi wa karibu miongoni mwa watumiaji wa twita wa Kiarabu. Kuanzia Saudi Arabia mpaka Palestina, watumiaji Twita wa Kiarabu wanajadiliana kuhusu mshikamano, kugawanyika na rasili mali za Sudani.

Syria: Propaganda ya Vyombo vya Habari vya Serikali Kuhusu Maandamano ya Tunisia na Misri

Mwanablogu wa ki-Syria Maurice Aaek amegundua[ar] kwamba vyombo vya habari vinavyoendeshwa na serikali nchini Syria vinachapisha habari za uongo na nusu-kweli kuhusu maandamano ya upinzani nchini Tunisia na Misri. Amegundua kwamba gazeti la Tishreen daily halikuweka sababu ambazo zilimfanya Ben Ali aondoke na kuwaachia watu wajitafsirie wenyewe, na kuwa gazeti...

Urusi: Mlipuko Katika Kiwanja cha Ndege cha Domodedovo

RuNet Echo  25 Januari 2011

Bomu lililipuka katika kiwanja cha ndege cha Domodedovo mjini Moscow, kwa uchache vifo vya kadri ya watu kumi vimeripotiwa. Mmiminiko wa Twita unapatikana hapa (RUS) na hapa (RUS, ENG). @ann_mint, ambaye anafanya kazi Domodedovo, alikuwa ni mmoja wa watumiaji wa kwanza wa Twita kuripoti juu ya mlipuko huo; “Kuna wahanga...

Sudan: Muda mfupi Kuelekea Kwenye Kura ya Maamuzi ya Sudani ya Kusini

Sudani ya Kusini itaendesha kura ya maoni ili kuamua ikiwa iendelee kubaki kuwa sehemu ya Sudani ama la ifikapo tarehe 9 Januari 2011. Kuna uwezekano ni mkubwa kuwa nchi hiyo kubwa zaidi katika bara la Afrika itagawanyika kuwa nchi mbili zinazojitegemea. Hapa ni maoni ya hivi karibuni zaidi kwenye makala za blogu kuhusu kura hiyo ya maoni. Southern Sudan will hold a referendum on whether or not it should remain as a part of Sudan on 9 January 2011. It is most likely that Africa's largest country will split into two. Here's our latest roundup of blog posts about the referendum. Southern Sudan will hold a referendum on whether or not it should remain as a part of Sudan on 9 January 2011. It is most likely that Africa's largest country will split into two. Here's our latest roundup of blog posts about the referendum.

Tunisia: Anonymous Dhidi ya Ammar – Nani Atashinda Vita ya Kuchuja Habari?

Kichuja habari cha Tunisia, kinachojulikana kama Ammar, kinaeendelea kutishia kuziharibu na kuzifunga anuani za wanaharakati wa mtandaoni, katika nchi hiyo ambayo imekuwa ikishuhudia wimbi la maandamano tangu katikati ya mwezi Desemba. Ni leo tu, wanaharakati wamedai kwamba serikali imeingilia anuani zao za barua pepe,na kuziingilia blogu na mitandao yao ya kijamii, na kuzizuia zisifanye kazi. Hatua hii inaonekana kuja kama kulipiza kisasi kwa shambulio lililofanywa na kikundi cha wanaharakati wa mtanda0ni wanaojulikana kama Anonymous, ambalo lililenga njia na mitandao ya muhimu ya Serikali ya Tunisia.

Kura ya Maoni ya Sudani Kusini 2011

Yaliyomo Habari Kusini mwa Sudan wakati Global Voices Habari zilizochaguliwa za Global Voices Rasilimali: Tovuti Twitter Facebook Videos Sudani Kusini ilianza kupiga kura ya maoni mnamo tarehe 9 Januari, 2011 ili kuamua kama waendelee kuwa sehemu ya Sudan kama sehemu ya Makubaliano ya Jumla ya Amani yaliyofanyika mwaka 2005 kati...