Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Novemba, 2012
Mkanganyiko wa Makubaliano ya OIC Kuanzisha Ofisi Nchini Myanmar
Shirika la Ushirikiano wa Kiislam (OIC) limependekeza kuanzisha ofisi nchini Myanmar kwa lengo la kukisaidia kikundi kidogo cha Waislamu nchini humo. Serikali ilishakubaliana na mpango huu lakini ilibadili uamuzi huu mara baada ya kutokea maandamano ya kupinga uamuzi huo katika maeneo mengi ya nchi.
Mwanzilishi wa Kikundi cha Kijeshi Kilichofutwa Nchini Pakistani Ajitolea Kuisaidia Marekani.
Wakati kukiwa na makelele na uharibifu mkubwa huko ukanda wa pwani ya mashariki mwa Marekani unaotokana na kimbunga kikubwa kijulikanacho kwa jina la Sandy, Hafiz Mohammad Saeed, mwanzilishi wa shirika la kijeshi lililofutwa la Lashkar e Taiba (LeT) na kiongozi wa Jaamat ud Dawa (JuD) ajitolea kutoa misaada ya kibinadamu kwa Marekani ili kufidia uharibifu.
Chile: Mahabusu wa Mapuche Wamaliza Mgomo wa Kutokula Uliodumu kwa Siku 60
Baada ya siku 60 za mgomo wa kutokula, mahabusu wanne wa Mapuche wamesitisha mgomo wao mara baada ya Mahakama Kuu ya Chile kukubaliana na baadhi ya madai yao. Juhudi hizi pia zimepelekea kuwepo kwa migowanyiko kiasi kuhusiana na mgogoro miongoni mwa watu wa Chile.
Uharibifu Nchini Syria Katika Picha
Wapiga picha wa Syria wanatumia mitandao ya kijamii kuweka taswira ya uharibifu katika maeneo mbalimbali na kwenye mitaa. Pamoja na ufinyu wa vitendea kazi vya utoaji wa habari, habari zinazotoka Syria zinaonesha hali ya kutisha ya uharibifu inayoikabili nchi ya Syria.
Mradi wa Tafsiri: Kauli ya Linda Uhuru wa Intaneti Ulimwenguni

Katika siku saba zijazo, Wafasiri wa Kujitolea wa Mradi wa Lingua wa taasisi ya Global Voices watakuwa wakitafsiri makala maalumu ambayo ni harakati ya utetezi unaofanywa na umma mtandaoni na...
Watoto wa Mitaani Bangladesh Wakabiliwa na Unyanyasaji
Jumla ya watoto wa mitaani nchini Bangladeshi wanakadiriwa kufikia 400,000. Karibu nusu ya idadi hiyo wanaishi katika Jiji la Dhaka. Asilimia kubwa ya watoto hao ni wasichana. Wasichana hao wa mitaani huishi katika mazingira yenye hatari nyingi hasa unyanyasaji na dhuluma nyingine.
Maelfu Watia Saini Pendekezo la Zawadi ya Nobel na Kusherehekea Siku ya Malala
Mwanaharakati wa elimu mwenye umri wa miaka 15 -- Malala Yousufzai -- aliyepigwa risasi mnamo tarehe 9 Oktoba 2012 na wanamgambo wa TTP, anaendelea kupata nafuu japo polepole. Mnamo tarehe 10 Novemba, watu kote ulimwenguni walimpongeza Malala kama kielelezo kwa ajili ya wasichana wapatao milioni 32 ambao hawapati fursa ya kwenda shulen.