Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Januari, 2013
Msumbiji: Uhamasishaji wa Kiraia Kuwasaidia Waathirika wa Mafuriko
Baada ya mvua kubwa iliyosababisha mafuriko kusini mwa Msumbiji yaliyowaacha maelfu ya raia bila makazi na wengi kupoteza maisha, kikundi cha kiraia cha Msumbiji Makobo kimeanza kampeni ya mshikamano inayoitwa...
Pasipoti za Kidiplomasia kwa Viongozi wa Kidini nchini Brazil?
Wizara ya Mahusiano ya Kimataifa ilitoa pasipoti za kidiplomasia kwa viongozi wa kanisa la kiinjili liitwalo World Church of the Power of God, hatua ambayo imewasha majadiliano makali kuhusu dhana ya nchi kutokuwa na dini kama inavyotamkwa katika katiba ya Brazili.
Uchafuzi wa Hewa wa Kutisha Jijini Tehran Waanikwa
Uchafuzi wa hewa umekuwa adui wa umma kwa mamilioni ya watu wa Tehran kwa miaka mingi sasa. Mapema mwezi huu, Wizara ya Afya ilitangaza kuwa, mwaka uliopita, zaidi ya watu 4, 400 walipoteza maisha kwa sababu ya uchafuzi wa hewa huko Tehran, mji mkuu wa Iran.
Jukwaa la Kiafrika Lenye Makala za Bure za Kitaaluma
Januari 24, ni siku ambayo inategemewa kuwa ya kuzindua rasmi Hadithi, ambalo ni jukwaa la kuhifadhia zana za bure za kitaaluma mjini Nairobi, Kenya. Wasomi mbalimbali na wadau wa mitandao watakusanyika...
“Wanasemaje Bamako?” Mazungumzo na Awa anayeishi Mali
Anne Morin na Awa Traoré wanabadilishana mawazo kuhusiana na maisha ya kila siku mjini Bamako, ujira usiokidhi mahitaji, gharama za maisha na hali ya kisiasa isiyotabirika wakati huu ambapo vita...
Wafalme Watatu Watembelea New York
Wafalme watatu walikuja na kuondoka, lakini siyo kabla ya kupita katika jiji la New York ili kusherehekea na mamia ya watoto waliojitokeza kwa ajili ya paredi. Shamra shamra hizi za Noeli, kwa karne nyingi, zimekuwa ni sehemu ya utamaduni wa watu wa Amerika wenye asili ya Karibeani na Walatini..The Three Kings came and went, but not before passing through New York City to celebrate with hundreds of children that came out for the parade. This Christmas celebration has been a part of the Caribbean and Latin American cultural traditions for numerous centuries.
Mwanaharakati wa Pakistani Khudi Ali Auawa Katika Mlipuko wa Bomu
Mnamo Januari 10, 2013 katika jiji la Quetta lililopo Kaskazini Mashariki mwa nchi ya Pakistani, watu 82 walipoteza maisha kwenye milipuko ya mabomu yaliyolenga eneo ambalo kimsingi lenye idadi kubwa ya Waislamu wa Shia jamii ya Hazara. Irfan Khudi Ali, mwanaharakati mashuhuri wa haki za binadamu ambaye bila kuchoka aliweka wazi uonevu wa kikabila unaofanywa kwa waShia wa Hazara nchini Pakistan, alifariki katika shambulio lililofuata. Kifo chake kimechochea watu kumpa heshima kwa juhudi zake kwa kuanzisha tena maandamano kupinga mauaji ya watu wa Shia nchini Pakistani.
Mashoga Washambuliwa Kaskazini mwa Kameruni
Oscarine Mbozo’a anaripoti [fr] katika blogu ya L'Actu kuwa shoga mmoja akiwa ameambatana na mwenzi wake walizomewa karibu na soko mnamo tarehe 6, Januari 2013, mjini Maroua, Kaskazini mwa Kameruni: Goche...