· Februari, 2013

Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Februari, 2013

Mgomo wa Nchi Nzima Wamshitua Rais wa Malawi

Rais wa Malawi Joyce Banda atupilia mbali shinikizo la kujiuzulu mara baada ya mamia ya maelfu ya wafanyakazi wa umma kuandamana kwa wiki mbili kuishinikiza serikali kuongeza mishahara, hali iliyopelekea kufungwa kwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Malawi na kusababisha hali ya taharuki mahospitalini na mashuleni.

Bulgaria: Pamoja na Serikali Kujiuzulu Maandamano Yapamba Moto

26 Februari 2013

Maandamano nchini Bulgaria yanaendelea: Ruslan Trad anataarifu kutoka mji mkuu wa Bulgaria kuwa, siku ya Jumapili, huko Sofia na katika majiji mengine, makumi ya maelfu ya watu waliandamana kupinga rushwa, gharama kubwa za huduma za jamii pamoja na umasikini.

Uhuru wa Vyombo vya Habari Nchini Myanmar Bado ni Giza

  25 Februari 2013

Uamuzi wa Myanmar wa kuivunja bodi katili ya ukaguzi ilisifiwa na makundi mbalimbali ya watu kama njia ya kuelekea kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini humo. Lakini, waangalizi wa uhuru wa vyombo vya habari waliainisha vitisho na mashambulio wanayokabiliana nayo waandishi wa habari wanaoishi nchini Myanmar.

Vurugu Zinazofadhiliwa na Serikali Nchini Angola

Mwanablogu Claudio Silva anaandika kwenye makala yake Africa Ni Nchi kwamba mtazamo wa kina juu ya vurugu zinazofadhiliwa na serikali (kufukuzwa watu mijini na kupigwa kwa waandamanaji) unahitajika ili kuelewa video mbili zilizosambaa sana mtandaoni na kuleta sintofahamu kubwa nchini (tazama habari maalumu za Global Voices). Anaandika “vurugu za Angola...

Bangladeshi: Raia Wakutana Kudai Haki Itendeke

  17 Februari 2013

Kidogo kidogo, makutano ya Shahbag katika mji mkuu wa Bangladesh, Dhaka yamefurika watu wenye lengo la kutaka haki kufuatia ukatili uliofanywa mnamo mwaka 1971 wakati wa harakati za vita vya kutafuta uhuru pamoja na kudai hukumu ya kifo kwa wahalifu wa vita.Drop by drop, the Shahbag intersection in Bangladesh's capital city Dhaka has become an ocean of people, demanding justice for the atrocities committed during the country's 1971 liberation war and death penalty for war criminals.

Udhaifu wa Watawala wa Afrika unajionesha Mali?

Ousmane Gueye katika tovuti ya Mondoblog anaandika [fr] kuhusu kuchelewa kupeleka vikosi vya kijeshi kasikazini mwa Mali: Kama tungekuwa tunasaiili matokeo ya watu wenye amani na huru kuingilia kati hali ya mambo nchini Mali, basi ni wazi kuwa kwa kuchelewa kupeleka vikosi vya ulinzi, nchi za Afrika zimewakosea wananchi wa Mali...