· Septemba, 2008

Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Septemba, 2008

Sheria inapokwaza haki za binadamu …

  29 Septemba 2008

Mtoto mwenye umri wa shule ya msingi aliyepatikana nje ya ndoa huko Zhuhai, kusini mwa China, hakubaliwi kujiunga na shule, kwa sababu mama yake hawezi kulipa faini kubwa ya kuwa na "mwana haramu", habari hii inasimuliwa na bloga, Han Tao.

Angola: Uchaguzi Katika Picha

  22 Septemba 2008

Waangola wako katika uchaguzi kwa mara ya kwanza katika miaka 16 - uchaguzi bado unaendelea Jumamosi hii katika vituo 320 jijini Luanda. Mpaka sasa, hakuna matukio yoyote yaliyoripotiwa, na moyo wa utu umedumu, kama ilivyoangaliwa na mpiga picha Jose Manuel da Silva.

Irani: Redio Zamaneh, Redio ya Mabloga

  21 Septemba 2008

Redio Zamaneh ni redio ya lugha ya kipersia yenye makao yake huko mjini Amsterdam. Zamaneh ni neno linalomaanisha “wakati” katika lugha hiyo. Redio Zamaneh (RZ) ni chombo huru cha utangazaji kilichosajiliwa kama asasi isiyo ya kiserikali huko Uholanzi, kikiwa na studio na makao yake makuu mjini Amsterdam. Mratibu wa redio...

Colombia: Watu Wanaswa na Mitego ya Upatu

  14 Septemba 2008

Kwa kupitia picha za video na mtandao wa marafiki wa Facebook, raia wa Colombia, Diego Alejandro, anaweka wazi udanganyifu na utapeli mkubwa uliojificha nyuma ya michezo ya upatu ambayo inatangazwa kama njia mbadala za uwekezaji. Katika nchi ambapo akaunti za benki zimepoteza maana kwa sababu ada za uendeshaji ziko juu kuliko riba anayopata mwenye akaunti, michezo hii ya upatu inayoshawishi kumjaza mtu mapesa, ambapo raia wanalipa kiasi fulani cha pesa ili kujiunga na kisha kuingiza marafiki zao 7 kabla wao hawajaanza kufurahia riba ya juu ajabu (kati ya asilimia 40 mpaka 70) basi imekuwa ni kivutio kikubwa mno.

Paraguai: Rais Lugo Kutopokea Mshahara

  12 Septemba 2008

Utawala wa Rais Ferdinand Lugo umeanza na tangazo kuwa hatapokea mshahara wake wa mwezi. "Sihitaji mshahara huo, ambao unapaswa kumilikiwa na masikini," alisema Lugo. Mabloga nchini humo wanatofautiana mitazamo, wakati mmoja anausifu uamuzi huo, mwingine anajiuliza ni vipi Rais lugo atajilipia gharama binafsi za maisha.

Nia ya Mwanablogu Mmoja Kumsaidia Mtoto Kamba huko Madagaska

Sauti Chipukizi  6 Septemba 2008

Ikiwa unataka kwenda sambamba na habari mpya mpya kutoka Madagaska, inawezekana kabisa ukawa ni msomaji wa Madagascar Tribune. Na kama wewe ni mdau wa gazeti hilo, hivi karibuni yawezekana ulishakutana na habari iliyoandikwa na mwandishi wa habari Herimanda R kuhusu upasuaji wa maradhi ya nadra na mafanikio yake ambao ulifanyika...

Venezuela: Wahindi wa Yukpa, Chavez na Mgogoro wa Ardhi

  6 Septemba 2008

Picha za video zinazotumwa kwenye mtandao wa internet na vyombo vya habari vya kiraia zinaonyesha yale yanayojiri kuhusu mgogoro unaoibuka nchini Venezuela kati ya Wahindi wa jamii ya Yukpa wanaoishi katika milima ya Perijá, wamiliki wa ardhi na Rais Chávez. Mgogoro huu kuhusu mipaka ya ardhi umekuwapo kwa takribani miaka 30, yaani tangu pale vikosi vya jeshi vilipowandoa kwa nguvu wanajamii wenyeji ya Ki-Yukpa na kuwapa ardhi hiyo wamiliki wapya walioanzisha mashamba makubwa ya mifugo, hasa ng'ombe, ambao wameendelea kuitumia ardhi hiyo tangu wakati huo.

Saudi Arabia: Kina Mama Huru

  6 Septemba 2008

WAKATI kukiwa hakuna shaka kwamba kuna vizuizi kwa wanawake waishio Saudi Arabia, havifanani na taswira iliyojengwa na wageni dhidi ya taifa hilo. Katika makala hii tunao ushauri kwa wakina mama wanaotaka kutembelea jiji la Jeddah wakiwa peke yao, kuna muhtasari wa hoteli za kina mama pekee jijini Riyadh, na wito kwa wageni wote wanajihisi kuzungumza kwa niana ya kina mama wanaokandamizwa wa Saudia.