Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Disemba, 2011
Dondoo za Video: Maandamano, Chaguzi, Utamaduni na GV
Baadhi ya habari za kuvutia za Global Voices na video za hivi karibuni kutoka Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, Mashariki na Ulaya Kati, Karibeani pamoja na Marekani ya Kusini, zimeletwa na Juliana Rincón Parra.
Global Voices: Changia Leo
2011 umekuwa mwaka usio wa kawaida katika maudhui ya mtandaoni. Global Voices imekuwepo pale wakati mapinduzi yalipotokea, wakati tawala za kidikteta zikianguka, na matokeo ya matumizi ya mtandao yaliposambaa katika miji na mitaa ya wachangiaji wetu wanaoripoti kutoka duniani kote.
Rwanda: Watumiaji wa Twita Wajadili Mpango wa Rais Kagame wa Kugombea Awamu ya Tatu
Wakati mjadala wa ikiwa katiba ya Rwanda ibadilishwe kuruhusu muhula wa tatu uanzidi kupamba moto, Rais wa Rwanda Paul Kagame asema raia wanao uhuru wa kusema kwamba wanamhitaji. Mwandishi wa Kiingereza Ian Birell alijibu kwenye twita akisema, “Hawako huru, na kwa kweli ndivyo ilivyo, kusema aondoke…
Uzbekistan: Mchezo wa Siasa katika Facebook
Facebook inaonekana kuanza kuchukua jukumu muhimu katika siasa za Uzbek. Hata hivyo , facebook ni imekuwa ni zaidi kwa ajili ya michezo na akaunti za kugushi kuliko chombo kuwa chombo cha harakati za kiraia. Ekaterina anaripoti.
Korea Kusini: Dikteta Kim Jong Il wa Korea ya Kaskazini afariki dunia
Kim Jong Il, dikteta wa Korea Kaskazini amefariki. Japokuwa kifo cha dikteta huyo mwenye sifa mbaya duniani ni jambo ambalo watu wanapaswa kulipokea vyema, watu wengi wa Korea Kusini wameonyesha wasiwasi juu ya hali tete katika bahari ya Korea itakayotokana na kifo chake cha ghafla.
Syria: Mwanablogu Razan Ghazzawi Ameachiwa HURU!
Habari zinasambaa mtandaoni kwamba mwanablogu wa Syria aliyekuwa gerezani anaweza kuachiwa huru wakati wowote kuanzia sasa. Ghazzawi, anayeblogu akiwa Syria kwa kutumia jina lake halisi, aliwekwa kizuizini akiwa njiani kuhudhuria warsha ya uhuru wa Vyombo vya habari iliyokuwa ikifanyika mjini Amman. Kuwekwa kwake kizuizini kulikosolewa na watumiaji wa mtandao, ambao sasa wanasubiri kwa hamu kuachiwa kwake. Amekuwa ndani kwa siku 15 sasa.
Mexico: Wanafunzi Wawili Wauawa Kwenye Maandamano Huko Ayotzinapa
Wanafunzi wawili, Jorge Alexis Herrera Pino na Gabriel Echeverría de Jesús, waliuawa tarehe 12 Desemba 2011, wakati wa maandamano ya wanafunzi wa shule ya vijijini ya Raúl Isidro huko Ayotzinapa, mji mkuu wa Guerrero, Chilpancingo, nchini Mexico. Mitazamo yenye utata kuhusu yalioyotokea imechapishwa mtandanoni.
Uarabuni: Hongera Tunisia!
Human rights activist Moncef Marzouki, 66, has been elected as Tunisia's new interim president today. His appointment, which was followed by a moving acceptance speech, was noted by netizens from across the Arab world, who cheered on Tunisia's progress towards democracy, wishing the same for their countries.
Iran: Yu Wapi Mwanafunzi Mwenzangu?
Several empty chairs in Iran's universities were formerly occupied by students who have now vanished or been expelled. This year Tahkim Vahdat, a leading student protest group, called for an “Empty Seat Campaign” on December 7 to remember the victims of religious and government repression in universities.
Zimbambwe: Hasira wakati Mzee Mugabe Anapowania Uchaguzi wa 2012
Chama cha ZANU –PF (Zimbabwe African National Union - Patriotic Front) kimempitisha Robert Mugabe kuwa mgombea wake kwa ajili ya uchaguzi wa rais unaotazamiwa kufanyika mwaka ujao. Kama uchaguzi utafanyika mwakani, Mugabe atakuwa na umri wa miaka 88 na atakuwa Mwafrika wa pili mzee zaidi kugombea katika uchaguzi wa rais. Kupitia Twita na Facebook wa-Zimbabwe wameonyesha hasira na kutokuamini kilichotokea.