Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Agosti, 2009
Mexico: Simulizi za Siri Kwenye Twita
Rafa Saavedra ni mtaalamu wa utamaduni wa chini chini kutoka mji wa Tijuana, Maxico. Katika mahojiano, anaelezea kila kitu kinachohusu mradi wake mmoja wa hivi karibuni unaojumuisha Twita na utoboaji wa siri.
Palestina: Maoni Juu ya Kuzinduliwa Kwa Huduma ya Google.ps
Google imeongeza anwani ya google.ps (google palestina) kwenye orodha yake zana inayotoa huduma za utafutaji zinazolenga sehemu mbali mbali. Anwani hiyo mpya inakusudiwa kufanya kazi katika ukanda wea Magharibi na Gaza, ambako watoaji huduma za intaneti hufanyia kazi zao.
Iangazeni Naijeria: Imetosha Sasa Basi
Pamoja na kuwa nchi yenye utajiri wa mafuta, hali ya ugavi wa umeme nchini Naijeria hairidhishi. “Katika sehemu nyingi za nchi, giza linatawala na majenereta yamechukua nafasi kama vyanzo vya nishati ya umeme” Inasema blogu ya Adebayo. Sasa Wanaijeria wameanzisha kampeni kubwa ya mtandao wa intaneti inayopinga hali hii inayogharikisha kwa kutumia tovuti za kijamii, hasa kwenye Twita kwa kutumia anwani ya #lightupnigeria (#iangazenaijeria).