Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Januari, 2013
Rais wa Chadi Awateua Wanawe Kushika Nafasi Nyeti
Djamil Ahmat anaripoti kuwa rais Déby wa Chadi amemteua mwanae wa kiume Mahamat Idriss Déby, 24, kuwa brigedia jenerali [fr] pamoja na maafisa wengine wanne. Tchadanthopus anaongeza kuwa mwanae mwingine Zackaria Idriss Deby alisemekana kukabidhiwa umakamu wa rais [fr] nafasi ambayo inampa madaraka yote wakati baba yake anapokuwa nje ya...
Kujitenga kwa Mtu wa Jamii ya Alawite: Jinsi Msichana wa Syria Alivyompoteza Mama Yake.
Loubna Mrie alipata pigo kubwa kutokana na msimamo wake kuhusiana na mapinduzi ya Syria. Kama mtu wa kikundi cha alawite aliyeamua kuwa na msimamo tofauti dhidi ya Rais Bshar Al Assad, aliamua kujitenga na jamii yake; watu
Mwaka Mpya na Mienendo ya Zamani Nchini Bahrain
Wakati nchi mbalimbali ulimwenguni kote zikiukaribisha mwaka mpya kwa fataki na shamrashamra, serikali ya Bahraini iliandaa utaratibu wa aina yake kwa waandamanaji nchini humo. kwa bahati, watumiaji wa mtandao wa intaneti walikuwa tayari, kuonesha na kuweka kumbukumbu ya baadhi ya matukio kwa ajili ya kushuhudiwa na sehemu nyingine yote ya ulimwengu.
Bangladeshi: Msichana Mwingine Mzawa Abakwa na Kisha Kuuliwa.
Kwa mara nyingine msichana mzawa ameuawa nchini Bangladesh baada ya kubakwa kikatili. Mhanga huyo, Khomaching Marma (14) alikuwa mwanafunzi wa darasa la nane. Ubakaji huu wa kikatili uliosababisha mauaji kwa mara nyingine tena umeamsha hasira na ghadhabu nchini kote. Watumiaji wa mtandao pia wanapinga vikali vitendo hivyo.
Mauritius na Visiwa vya Reunion Kukumbwa na Kimbunga Dumile
Lexpress.mu linaripoti kwamba Mauritius iko kwenye hatari kubwa [fr] kufuatia kisiwa hicho kunyemelewa na uwezekano wa Kimbunga cha Dumile. Kisiwa cha Agaléga cha nchi hiyo kiliathiriwa vibaya na kimbunga hicho [fr] na nishati ya umeme ulikatika kwa masaa 24. Kisiwa cha Réunion pia kiko kwenye hatari kubwa [fr].
Watu 60 Wauawa kwa Msongamano nchini Abidjan
Magogo ya miti yaliyokuwa yameanguka barabarani yanaonekana kusababisha msongamano mkubwa na ulioua watu 60 na kujeruhi wengine 49 wakati wa sherehe za kuukaribisha mwaka mpya mjini Abidjan, Côte d'Ivoire. Kutokana na ukweli kuwa eneo hilo halikuwa na mwanga wa kutosha inawezekana ndio sababu iliyochangia tukio hilo la msongamano ulisababisha mkanyagano...
Kusherehekea Mwaka 2012 na Sauti za Dunia
Kadiri mwaka 2012 unavyofikia tamati, tungependa kutoa shukrani zetu kwa kazi nzuri, ubunifu pamoja na kuonesha kujali mambo mengi katika jumuia ya Sauti za Dunia. Mwaka 2012 umekuwa ni mwaka wa ukuaji wa kasi kabisa na wa mafanikio kwa Sauti za Dunia ( Global Voices). Yafuatayo ni baadhi tu ya mafanikio:
Kuhusiana na Vuguvugu la Mabadiliko ya Umma
Gaurav Mishra anachambua nguvu ya vuguvugu la mabadiliko linaloanzia kwa watu wa kawaida na namna inavyofanya kazi kuleta mabadiliko chanya katika utendaji wa vyombo vikuu vya habari kwa kutumia vyombo vya habari vya kiraia.
Hakuna Usalama kwa Waandishi wa Kiraia Nchini Bahrain
Baada ya video ya "kibao" cha polisi wa Bahrain kusambaa sana mtandaoni, Waziri wa Mambo ya Ndani alitoa tamko akiomba kuwa yeyote aliyepiga picha tukio hilo aliripoti haraka kwa mamlaka zinazohusika. Siku mbili baadae, na kinyume na kauli hiyo, watu wengi walishangazwa na kukamatwa kwa mpiga picha.
Waandamanaji wa Hangari Wafunga Daraja, Wanafunzi Watatu Watiwa Nguvuni.
Harakati za maandamano ya wanafunzi zinaendelea nchini Hangari. Usiku wa Jumatano, waandamanaji walizingira daraja la Budapest na wanafunzi watatu waliishia kuwekwa kizuizini na polisi.