Habari kuhusu Uandishi wa Habari za Kiraia kutoka Disemba, 2009
Brazil: Wito wa Kugomea Gazeti Linaloongoza Nchini
Wanablogu wa Brazili wamekuwa wakihamasisha mgomo dhidi ya kile walichokiita Coupist Press Party, yaani Sherehe ya Chombo cha Habari ya Kutaka Kupindua Serikali, kwa hiyo wamekuwa wakiwataka watu kuacha kununua, kusoma au kutoa maoni na badala yake kufuta usajili wao kutoka kwenye gazeti la Folha de São Paulo na tovuti yake.
Ghana: Rais Atta Mills Dhidi ya Chama Chake Mwenyewe?
Katika miezi michache kuelekea uchaguzi wa Rais Hohn Evans Atta Mills, wa-Ghana wengi, pamoja na wale walio nje ya nchi, waliohofu kwamba ushindi wa chama cha New Democratic Congress (NDC) ungeweza kugeuka kuwa utawala mwingine wa mwanzilishi wa chama hicho na mtawala wa zamani wa kijeshi, Rais Jerry John Rawlings.
Morocco: Kusherehekea Idi katika Sehemu za Mashambani
Wikiendi hii iliyopita, Wamoroko walisherehekea Eid Al-Adha. Wanablogu walioko sehemu za vijijini nchini Moroko wanasimulia simulizi zao kuhusu Eid ya mwaka huu. Kwa kuwa upatikanaji wa intaneti upo sehemu chache n amara nyingi ni wa aghali mno nje miji mikubwa, wengi wanaoblugu kutokea sehemu za mashamba ni Wafanyakazi wa Amani wa Kujitolea (PCVs) na kwa hiyo wako katika nafasi ya kuweza kutoa mitazamo kama wageni kutoka nje… walioko ndani.
Austria: Jinsi Nyenzo Za Habari Za Kijamii “Zinavyoviwashia Moto Vyuo Vikuu”
Je, ulijua kwamba katika wakati huu vyuo vikuu vingi kote Ulaya vinakaliwa na wanafunzi? Vuguvugu hili lote limeratibiwa kwa kutumia nyenzo za uanahabari wa kijamii katika mtandao.
Namibia: Nafasi ya Vyombo Vipya vya Habari kwa Uchaguzi wa 2009
Uchaguzi wa rais na bunge la taifa la Namibia ulifanyika tarehe 27 na 28 Novemba 2009. Vyama vya siasa na mashirika yasiyo ya kiserikali yalitumia nyenzo kadhaa za habari za kijamii kupiga kampeni, kufuatilia na kuripoti Uchaguzi.
China: Uvunjaji Nyumba kwa Kutumia Mabavu
Visa viwili vya uvunjaji nyumba kwa mabavu vimeibua hisia za kutaka kulindwa zaidi kwa haki za raia na utatuzi wa migogoro nchini Uchina. Watumiaji wa mtandao wa Kichina wanatoa maoni.
Warsha ya Wanablogu wa Uarabuni: Tafakuri ya Twita kwa Siku ya Kwanza
Wakati siku ya kwanza ya Warsha ya Pili ya Mwaka ya Wanablogu wa Uarabuni ikifungwa, tutaangalia tafakuri za washiriki kwa siku nzima, kujua wamejifunza nini na namna wanavyojisikia. Siku ilianza kwa kishindo, wakati waandaaji wa Global Voices Sami ben Gharbia, Amira Al Hussaini, na wafadhili wetu kutoka Mfuko wa Heinrich...
Indonesia: Sarafu za Kudai Haki
Raia wa mtandaoni (Netizens) wamezindua kampeni ya kukusanya fedha zilizo katika muundo wa sarafu ili kumuunga mkono Prita Mulyasari, mama wa nyumbani raia wa Indonesia aliyeandika malalamiko yake mtandaoni dhidi ya hospitali iliyotoa huduma mbaya, na ambaye alipatikana na hatia na mahakama moja ya kosa la "kuchafua jina" la hospitali hiyo binafsi.
Thailand: Waziri Mkuu wa Zamani Afariki Dunia
Samak Sundaravej — Gavana wa Zamani wa Bangkok, mwendeshaji wa kipindi cha mapishi, na Waziri Mkuu wa 25 wa Thailand amefariki dunia tarehe 24 Novemba. Soma maoni ya wanablogu na wanatwita wa Bangkok
Mwanamuziki mmoja wa Afrika Mashariki awashinda wengine wote kwa umaarufu wa mtandaoni duniani
Si wengi wanamfahamu kama Mwanaisha Abdalla bali Nyota Ndogo, ni jina linalojulikana kwenye kila nyumba katika Afrika Mashariki. Amekuwa akikusanya mashabiki wa mtindo wake wa kipekee wa Afrika Mashariki kwa miaka zaidi ya 4 sasa. Blogu yake, katika upande mwingine, imekuwa ikiendeshwa kwa muda wa miaka 3. Hapana shaka kuwa blogu hiyo imechangia ongezeko la kambi ya mashabiki kwenye mtandao wa intaneti.