Habari Kuu kutoka Disemba 2011
Habari kutoka Disemba, 2011
Uzbekistan: Mchezo wa Siasa katika Facebook
Facebook inaonekana kuanza kuchukua jukumu muhimu katika siasa za Uzbek. Hata hivyo , facebook ni imekuwa ni zaidi kwa ajili ya michezo na akaunti za kugushi kuliko chombo kuwa chombo cha harakati za kiraia. Ekaterina anaripoti.
Korea Kusini: Dikteta Kim Jong Il wa Korea ya Kaskazini afariki dunia
Kim Jong Il, dikteta wa Korea Kaskazini amefariki. Japokuwa kifo cha dikteta huyo mwenye sifa mbaya duniani ni jambo ambalo watu wanapaswa kulipokea vyema, watu wengi wa Korea Kusini wameonyesha wasiwasi juu ya hali tete katika bahari ya Korea itakayotokana na kifo chake cha ghafla.
Syria: Mwanablogu Razan Ghazzawi Ameachiwa HURU!
Habari zinasambaa mtandaoni kwamba mwanablogu wa Syria aliyekuwa gerezani anaweza kuachiwa huru wakati wowote kuanzia sasa. Ghazzawi, anayeblogu akiwa Syria kwa kutumia jina lake halisi, aliwekwa kizuizini akiwa njiani kuhudhuria warsha ya uhuru wa Vyombo vya habari iliyokuwa ikifanyika mjini Amman. Kuwekwa kwake kizuizini kulikosolewa na watumiaji wa mtandao, ambao sasa wanasubiri kwa hamu kuachiwa kwake. Amekuwa ndani kwa siku 15 sasa.
Mexico: Wanafunzi Wawili Wauawa Kwenye Maandamano Huko Ayotzinapa
Wanafunzi wawili, Jorge Alexis Herrera Pino na Gabriel Echeverría de Jesús, waliuawa tarehe 12 Desemba 2011, wakati wa maandamano ya wanafunzi wa shule ya vijijini ya Raúl Isidro huko Ayotzinapa, mji mkuu wa Guerrero, Chilpancingo, nchini Mexico. Mitazamo yenye utata kuhusu yalioyotokea imechapishwa mtandanoni.
Uarabuni: Hongera Tunisia!
Human rights activist Moncef Marzouki, 66, has been elected as Tunisia's new interim president today. His appointment, which was followed by a moving acceptance speech, was noted by netizens from across the Arab world, who cheered on Tunisia's progress towards democracy, wishing the same for their countries.
Iran: Yu Wapi Mwanafunzi Mwenzangu?
Several empty chairs in Iran's universities were formerly occupied by students who have now vanished or been expelled. This year Tahkim Vahdat, a leading student protest group, called for an “Empty Seat Campaign” on December 7 to remember the victims of religious and government repression in universities.
Zimbambwe: Hasira wakati Mzee Mugabe Anapowania Uchaguzi wa 2012
Chama cha ZANU –PF (Zimbabwe African National Union - Patriotic Front) kimempitisha Robert Mugabe kuwa mgombea wake kwa ajili ya uchaguzi wa rais unaotazamiwa kufanyika mwaka ujao. Kama uchaguzi utafanyika mwakani, Mugabe atakuwa na umri wa miaka 88 na atakuwa Mwafrika wa pili mzee zaidi kugombea katika uchaguzi wa rais. Kupitia Twita na Facebook wa-Zimbabwe wameonyesha hasira na kutokuamini kilichotokea.
Zambia: Magari Mapya ya Kifahari ya Mtoto wa Rais Yasababisha Minong’ono
Taarifa zilizotangazwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya Kiraia ya Committee of Citizens, Gregory Chifire, kwamba mtoto wa kiume wa rais wa Zambia, Mulenga Sata, hivi karibuni alijipatia magari mawili ya kifahari, zimevutia hisia mchanganyiko kutoka kwa wa-Zambia watumiao mtandao
Kongo (DRC): Wakongo Waishio Nje ya Nchi Walipuka Kumpinga Kabila
Wakati Kongo (DRC) ikingoja matokeo ya mwisho ya kura za Urais na wabunge, wa-Kongo waishio nje ya nchi hiyo, ingawa hawakuruhusiwa kupiga kura, wameonyesha kujitolea kwako kwa kuzifanya sauti zao zisikike. Julie Owono anataarifu.
Tanzania: Zinavyosema Blogu na Twita Katika Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania
Desemba 9, 2011, ni siku maalumu kwa Watanzania wakati Tanganyika, ambayo ni sehemu ya Muungano wa Tanzania ikitimiza miaka 50 ya uhuru. Katika mtandao, wanablogu na watumiaji wa twita wanasherehekea na kutafakari kwa kina mustakabali wa Tanzania.