Habari Kuu kutoka Mei 2013
Habari kutoka Mei, 2013
Lebanon: Mwanablogu Apata Kipigo kwa Kupiga Picha
Mwanablogu wa ki-Lebanoni Habib Battah anaeleza namna alivyoshikiliwa bila hiari, akilazimishwa kufuta picha katika kamera ya simu yake na kudhalilishwa mfululizo katika posti hii inayohusiana na ripoti ya Beirut. Aliporipoti suala hilo katika kituo cha polisi mahali alipokuwa, mafisa wanaohusika walimkana na kumgeuzia kibao yeye. Anaongeza: Walikuwa sahihi. Kama watu...
Wafanyakazi Wavamia Majengo ya Serikali Nchini Mauritania
Siku ya Jumanne asubuhi, Mei 28, 2013, maelfu ya vibarua, wanaolipwa ujira wao kwa kufanya kazi kwa siku, walianzisha maandamano makubwa [ar] huko Zouérat, mji mkuu wa jimbo la Tiris Zemmour kasikazini mwa Mauritania, wakidai mikataba inayoeleweka na haki zao nyinginezo ikiwa ni pamoja na kumalizwa kwa ukiritimba wa wafanyabiashara...
Je, Baada ya miaka 50, Chama Tawala cha Malaysia Kitashinda Uchaguzi?
Malaysia wnaajiandaa kwa uchaguzi mkuu wa 13 utakaofanyika Mei 5. Maudhui yanayotawala duru za kampeni za uchaguzi huo ni matarajio makubwa waliyonayo wananchi, au 'ubah' kwa lugha ya wenyeji. Je Chama tawala cha Barisan Nasional, kilichokaa madarakani kwa miaka 50, kitaendelea kutawala nchi hiyo?
Kwa nini Mashirika ya Umma Yameshindwa Nchini Zambia
Elias Munshya, mwanasheria na mchungaji wa Zambia, anaeleza kwa nini mashirika ya umma yamedumaa nchini Zambia tangu uhuru: Mashirika ya umma hayajawahi kutengeneza faida tangu mwaka 1964. Yamekuwa yakiendeshwa kiholela bila utaalamu wa kibiashara bali kisiasa. Mashirika haya hayajawahi kuwa na wataalamu wanaoendesha bodi husika bali yamejaa wafanyakazi kwa misingi...
Botswana: Kuibwa kwa Kazi ya Sanaa ya “Bushman's Secrets”
MyWeku anaichambua filamu yenye maudhui halisi (documentary) inayoelezea wizi wa kazi ya sanaa ya Sana iitwayo “Bushman's secrets”: Filamu hii inachora picha inayosikitisha ya namna ambavyo Uniliver, kampuni inayojinadi kama “mzalishaji mkubwa tena nambari moja duniani wa barafu zitengenezwazo kwa maziwa maarufu kama ice cream,” sasa linatumia bila aibu maudhui...
Jamhuri ya Dominika: Mwanafunzi Auawa kwenye Maandamano
Mnamo siku ya Alhamisi ya tarehe 8 Novemba, 2012, Chuo Kikuu cha Santo Domingo kiligeuka kuwa uwanja wa maandamano yanayopinga mpango wa serikali kubana matumizi. Wakati wa maandamano, polisi walisababisha kifo cha mwanafunzi wa udaktari mwenye miaka 21, William Florián Ramírez. Haikuchukua muda mrefu sakata hilo lilihamia katika mitandao ya kijamii.
Rais wa Chama cha Madaktari Msumbiji Akamatwa
Baada ya mgomo wa madaktari uliodumu kwa takribani juma moja nchini Msumbuji, Dr. Jorge Arroz, Rais wa Associação Médica de Moçambique, amekamatwa usiku wa Jumapili, Mei 26, 2013, kwa tuhuma za “uchochezi” (kuhamasisha watu kutokuridhishwa au kuiasi serikali). Kwenye mtandao wa Twita na Facebook, @verdademz, @canal_moz na ripoti nyingine za...
Saudi Arabia Yawanyonga Raia Watano wa Yemeni na Kutundika Miili Yao Hadharani
Raia watano wa Yemeni waliotiwa hatiani kwa mauaji na ujambazi walinyongwa kwa kukatwa kichwa nchini Saudi Arabia na miili yake kuanikwa hadharani huko Jizan, mji ullio kusinimagharibi mwa nchi hiyo. Picha za miili hiyo ikining'inia kwenye kamba hewani ilisambaa kwenye mtandao wa Twita na facebook kama hatua ya wa-Yemeni kupinga ukatili huo.
Rafael Correa Aapishwa kwa Kipindi cha Tatu Kama Rais wa Ekuado
Rafael Correa ameapishwa kuingia ikulu kama Rais wa Jamhuri ya Ekuado kutawala mpaka 2017..
Shambulio la Mabomu Mawili ya Kujitoa Muhanga Nchini Niger Yaua Watu 23
Benjamin Roger wa Jeune Afrique anaripoti [fr] kuwa wanajeshi 18, raia mmoja na magaidi wanne waliuawa mapema subuhi ya leo katika shambulio la mabomu ya kujitoa Muhanga kwenye gari mjini Agadez, Niger tarehe 23 Mei. Anaongeza kuwa wanafunzi wa chuo cha kijeshi wametekwa na gaidi mwingine kufuatia mabomu hayo. Wakati...