Mei, 2009

Habari kutoka Mei, 2009

Tajiri Wa Kimisri Ahukumiwa Kifo

Wamisri walishuhudia hukumu isiyotarajiwa katika historia ya vyombo vya sheria nchini humo: Bilionea Hesham Talaat Moustafa, pamoja na mamluki wake (mpiga risasi wa kukodi) Mohsen El Sokari wamehukumiwa adhabu ya kifo kutokana na kuhusika kwao katika mauaji ya mwimbaji wa Kilebanoni Suzanne Tameem. Mauaji hayo ya kinyama yalitokea huko Dubai, UAE, na hukumu iliyotolewa Alhamisi imesababisha mshtuko na mshangao wakati wanablogu walipojaribu kukubaliana na yaliyotukia.

Uchaguzi wa India 09: India Imepiga Kura, Imeamua kuimarisha Utulivu

  20 Mei 2009

Matokeo ya Uchaguzi yanamiminika kutoka kila upande wa nchi na ni dhahiri kwamba India imepiga kura kwa kishindo ili kuchagua serikali imara ya mseto ya UPA, chini ya uongozi wa chama cha Congress. Dr Manmohan Singh atakuwa Waziri Mkuu kwa mara ya pili mfululizo. Hata kabla matokeo hayajatimia, kwa kuangalia tu mwelekeo, kundi la vyama vya mseto la NDA linaloongozwa na chama cha BJP limetangaza rasmi kushindwa kwake katika uchaguzi.

Sri Lanka: Wanablogu Watathmini Kifo cha Kiongozi wa LTTE

  19 Mei 2009

Serikali ya Sri Lanka imetangaza kwa kupitia vyombo vya habari vya taifa pamoja na ujumbe wa simu za mkononi mchana leo (Jumatatu, 18 Mei, 2009) kwamba kiongozi wa Kundi linalotaka kujitenga la Wa-Tamil, the Liberation Tigers of Tamil Eelam (LTTE), Vellupillai Prabhakaran, amefariki. Salamu za rambirambi zinaashiria kwamba alikuwa shujaa kwa baadhi ya watu kadhalika wengine walimchukulia kama muuaji katili. Wanablogu wa Ki-Sri Lanka wanatathmini urithi wa kiongozi huyu wa vita na maana ya kifo chake kwa mustakabali wa Watamil na watu wa Sri Lanka.