Habari kutoka Aprili, 2013
Ujasiriamali,Utamaduni na Mshikamano katika Afrika
Pamoja na ukuaji mkubwa wa kiuchumi, bara la Afrika bado linahangaika kukuza kada ya wajasiriamali wazawa watakaoweza kudhibiti viwanda vya kimkakati. Wasomi na watafiti wengi wa ki-Afrika wanajaribu kuelewa atahri za tabia za kimila katika ujasiriamali barani humo.
Uganda: Kukumbuka milipuko ya mabomu ya 2010
Wananchi wa Uganda wameutumia mtandao wa Twita na Facebook kuwakumbuka wahanga 2010 wa milipuko yha mabomu iliyotokea kwenye klabu ya Rugby huko Kyaddondo na katika baa ya Kijiji cha Kiethiopia jijini Kampala Uganda.Mashambulizi hayo yalitokea wakati ambao wapenzi wa kandanda walikuwa wakitazama mpambano wa fainali kati ya Uhispania na Uholanzi uliofanyika nchini Afrika Kusini.
Jaribio la Mapinduzi katika Visiwa vya Comoro
Jeshi la Pilisi nchini Comoro limesema linawashikilia watu wanaosemekana kuwa wahaini raia wa Kongo na Chadi kwa tuhuma za jaribio la kuiangusha serikali lililofanyika mwisho wa wiki. Linfo.re anaongeza kwamba...
Washindi wa Tuzo za Kwanza za Uandishi wa Kiraia Nchini Ghana
Tumepata matokeo ya Tuzo za kwanza kabisa za Uandishi wa Kiraia nchini Ghana.
Iran: Wakati Matetemeko yanaua, “Televisheni Zinafundisha Sala”
Matetemeko makubwa mawili ya ardhi yalilitikisa eneo la kaskazini magharibi nchini Iran, Mashariki jimbo la Azarbaijan mnamo Jumamosi (Agosti 11, 2012), na kuua watu 250 na kujeruhi karibu 1800. Matetemeko ya ardhi kipimo cha 6.4 na 6.3 katika ukubwa, na kusababisha uharibifu mkubwa na mateso. Wa-Irani waliingia kwenye mtandao wa intaneti ili kuwaombolezea wahanga na kuomba watu kujitolea damu na msaada. Pia walionyesha hasira zao kwa televisheni ya kitaifa ya Iran, ambayo hutangaza vipindi vya dini, badala ya kutoa taarifa kwa watazamaji kuhusu matetemeko ya ardhi na jinsi ya kusaidia.
Misri: Mubarak ahukumiwa kifungo cha maisha
Dunia ilishuhudia wakati mahakama ya Misri ilipomhukumu aliyekuwa Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak na Waziri wake wa Mambo ya Ndani Habib Al Adly kifungo cha maisha hivi leo kufuatia kukutwa na hatia ya kuhusika na mauaji ya waandamanaji. Hukumu hiyo ilifikiwa baada ya vikao 49, masaa 250, na kuandikwa katika kurasa 60,000.
Uturuki: Polisi Watumia Mabomu ya Machozi Kuwatawanya AkinaMama Waandamanaji
Wafungwa wa kisiasa wa Kikurdi wamefikia siku yao ya 55 ya mgomo wa kula. Kuna mamia ya wafungwa wa kisiasa walio kwenye mgomo wa kula nchini Uturuki, na hii imesababisha maandamano mshikamano katika bara la Ulaya, na hususani ndani ya Uturuki. Mapema jana [4 Novemba 2012], wanawake ambao ni mama wa baadhi ya wafungwa wa kisiasa walifanya maandamano ya kukaa, na walijikuta wakipambana na mabomu ya machozi, pamoja na kunyunyuziwa maji ya kuwasha. Wa- Kurdi duniani kote wanapinga kimya kinachotumika kushughulikia adha yao.
Asasi za Kiraia za Urusi “Zakaguliwa” na Mwendesha Mashitaka

Wanaharakati wa DemVybor katika jiji kuu la eneo la Voronezh waliripoti kwenye blogu ya DemVybor[ru] kwamba Asasi Zisizo ki-Serikali zinakaguliwa na ofisi ya mwendesha mashitaka wa umma wa jiji hilo. Mashirika...
Syria: Kutwiti Kutokea Vitani Jijini Aleppo
Mwandishi wa Habari Jenan Moussa amerudi mjini Aleppo, nchini Syria, akitwiti tajiriba yake wakati vita kati ya vikosi vinavyopinga serikali na vile vinavyoiunga mkono serikali inavyozidi kushika kasi. Twiti za Moussa ni za kawaida na za kibinafsi sana, zikiwapa wasomaji wake taswira ya maisha yalivyo kwa wale walio kwenye uwanja wa vita.
AZISE ya Uwazi Yajiandaa kwa Uchaguzi wa Jumapili Nchini Venezuela
Wakati wapiga kura wa Venezuela wakijiandaa kuelekea kwenye uchaguzi wa mara ya pili katika kipindi cha miezi sita, kikundi cha Asasi Zisizo za Kiserikali kimekusanya nguvu ili kuhakikisha kuwa wanakuza uwazi katika mchakato wa uchaguzi.