Oktoba, 2010

Habari kutoka Oktoba, 2010

Irani: Ziara ya Rais Ahamdinejad Nchini Lebanoni

Rais wa Irani, Mahmoud Ahmadinejad, amemaliza ziara yake ya siku mbili nchini lebanoni. Ilikuwa ni ziara yake rasmi ya kwanza tangu mwaka 2005 wakati alipochukua madaraka. Alikuwa na mazungumzo na maofisa wa Lebanoni na alizuru ngome za maswahiba wa Irani. Alipata mapokezi ya shujaa. Wanablogu kadhaa wa Irani walitoa maoni kuhusu ziara hiyo.

Urusi: Wanablogu wakutana na Balozi wa Irani, waepa kuhoji masuala nyeti

Mkutano kati ya wanablogu wanaoongoza nchini Urusi na Balozi wa Irani jijini Moscow, siku tatu tu baada ya mwanablogu Hossein Derakshan kuhukumiwa kifungo cha miaka 19.5 jela kwa kile kilichoelezwa kuwa ni "kufanya propaganda zinazoipinga serikali" ulizionyesha wazi juhudi zisizoeleweka za diplomasia ya mtandaoni ya Irani nchini Urusi. Vilevile ulionyesha jinsi maslahi binafsi ya kibiashara pamoja na mtizamo taharuki uliopita kiasi wa baadhi ya wanablogu maarufu wa Urusi.

Tanzania: Matumizi ya Vyombo vya Habari vya Kijamii kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2010 Nchini Tanzania

Tanzania inaelekea katika uchaguzi wake mkuu mnamo Oktoba 31 mwaka huu na hivi sasa kampeni za uchaguzi zinaelekea kileleni. Wakati kampeni zikipamba moto, wagombea wa nafasi ya urais, ubunge na udiwani wameanza kutumia zana mpya za mawasiliano ya jamii ili kuwasiliana na wapiga kura. Sanjari na mikutano ya kampeni, ambayo hulenga watu wengi zaidi, idadi ndogo ya wanasiasa wameanza kutumia zana za mawasiliano ya kijamii kama vile blogu, picha za video za mtandaoni, Facebook na Twitter ili kukuza mawasiliano na wapiga kura.