Habari Kuu kutoka Novemba 2009
Habari kutoka Novemba, 2009
Malawi: Rais Ataka Nguvu Zaidi
Rais wa Malawi ataka nguvu zaidi!: “rais wa Malawi Bingu wa Mutharika, ambaye chama chake kina wabunge wengi katika bunge, anataka kunonesha nguvu zake kabla hajatoka kwenye ulingo wa siasa mwaka 2014.”
Somalia: Kuufahamisha mtandao wa waandishi na wanablogu wa Kisomali
Kituo cha habari cha Somalia ni jukwaa la waandishi na wanablogu wa Kisomali wanaoishi ndani na nje ya Somalia. Kituo kinasambaza machapicho ya habari na kuchapisha blogu zilizoandikwa na waandishi wa habari.
Afrika: Haki za Wanawake
Sokari anaandika kuhusu Toleo Maalum la Masuala ya Wanawake la Pambazuka linaloangalia miaka 15 iliyopita tangu mkutano au Jukwaa la Vitendo mjini Beijing pamoja na mustakabali wa haki za wanawake barani.
Brazil: Mtazamo wa Wakazi wa Vitongoji Maskini
Katika makala hii, tunasikia mitazamo ya wanahabari raia kutoka mradi wa Viva Favela kuhusiana ya vurugu inayotokana na mihadarati huko Rio de Janeiro na jinsi inavyofagia makazi ya walalahoi, kama wanavyoiona mbele ya milango ya nyumba zao.
Azerbaijan: Baada ya Hukumu ya Wanablogu wa Video
Siku chache baada ya hukumu ya vijana wanaharakati wawili wa blogu za video huko Azerbaijan, wanablogu wengine wanaanza kuongea kwa sauti juu ya kifungo cha Adnan Hajizade na Emin Milli. Wanaharakati hawa wa mtandaoni watatumikia vifungo vya miaka miwili na mwingine miaka miwili na nusu gerezani baada ya mashitaka ambayo...
Ufaransa: Tuzo ya Fasihi Yaja na Masharti
Mwanzo wa msimu wa Fasihi ya Kifaransa mwaka huu ulishuhudia mwandishi wa riwaya na michezo ya kuigiza mwenye asili ya Kisenegali na Kifaransa Marie N’Diaye akipewa tuzo iliyosuburiwa sana ya Prix Goncourt. Lakini, N’Diaye na familia yake walikwishahamia mjini Berlin miaka miwili iliyopita, hasa kutokana na siasa za rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy. Mwaka jana, jopo la tuzo hii yenye hadhi walizusha hisia kali pale walipomchagua mwandishi wa Kiafghani Atim Rahimi, kwa kitabu chake cha Kifaransa, Syngué Sabour. Je hii itakuwa ni fursa nyingine ya kusherehekea mchanganyiko wa aina mbalimbali katika jamii inayobadilika ya Kifaransa? Au itakuwa ni wasaa utakaoharibiwa na utete wa tukio?
China: Obama ni Mshabiki Mkubwa wa Kutokuchuja Habari
Adam Minter amesikitishwa na maoni ya Obama kwenye Mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Shanghai, hasa, maelezo yake kuwa “Mimi ni muunga mkono mkubwa wa kutokuchuja habari“.
Paraguay: Wenyeji Wanyunyiziwa Dawa za Kuua Wadudu kwa Ndege
Huko Mashariki mwa Paraguay, jumla ya watu 217 wa jumuiya ya wenyeji ya Ava Guaraní walianza kusumbuliwa wakionyesha dalili mbalimbali za kiafya zinazoaminika zilisababishwa na unyunyiziaji wa makusudi wa dawa za kuua wadudu hasa baada ya wao kuwa wamegoma kuhama kutoka katika ardhi waliyoirithi kutoka kwa mababu zao.
Karibea: Tuzo za Fasihi ya Kifaransa
Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, katika makala hii kutoka Haiti, na hii kutoka Guadeloupe na hii...
Finland: Suala la Lugha
Nordic Voices anaandika kuhusu ‘suala la lugha” huko Finland.