Aprili, 2009

Habari kutoka Aprili, 2009

Paraguai: Rais Lugo Akiri Kuzaa Mtoto Wakati Bado Akiwa Askofu

  19 Aprili 2009

Hivi karibuni Rais wa Paraguai Fernando Lugo alikiri kuwa alizaa mtoto wakati alipokuwa askofu wa kanisa la Katoliki la Roma. Habari hii imesababisha utata kati ya wanasiasa, vyombo vya habari, na wanablogu ambao wanaandika kuhusu kusikitishwa kwao na kiongozi huyo, na kadhalika jinsi ambavyo kuna matatizo mengine makubwa zaidi yanayotisha ambayo yanapaswa kutiliwa mkazo ikilinganishwa na vitendo vinavyofanywa na wanasiasa wengine.

Irani: Mwaka Mpya Waanza na Ujumbe Kutoka Kwa Obama

  10 Aprili 2009

Siku Wairani waliposherehekea Norouz (Nowruz) kama sikukuu ya mwaka mpya nchini Irani, raisi wa Marekani Barak Obama alituma ujumbe kwa watu wa Irani na kwa viongozi wa Jamhuri ya kiislamu, ujumbe huo ulitoa rai ya kutaka mwanzo mpya kati ya nchi hizo mbili. Wanablogu kadhaa wametoa maoni kuhusu ujumbe huo, angalia baadhi ya maoni hayo.