Habari Kuu kutoka Disemba 2009
Habari kutoka Disemba, 2009
Je, China Iliharibu Makubaliano ya Copenhagen?
Uln alijaribu kuchambua ni nini kilichotokea Copenhagen na kuhoji kwa nini nchi zinazoendelea hazikusaini baina yao wenyewe makubaliano ya kupunguza utokaji wa gesi ya ukaa. Inside-Out China ametafsiri taarifa inayosimulia habari kutoka kwa walio ndani kuhusu mienendo ya Wen Jiabao kule Copenhagen.
Msumbiji: Je, ni Lugha Ngapi Zinazungumzwa Nchini?
Kuna lugha 20 zinazozungumzwa nchini Msumbiji, kwa mujibu wa tovuti ya serikali, zaidi ya lugha ya serikali ya Kireno. Carlos Serra [pt] anajiuliza kama kuna lugha nyingine zaidi, kwa mujibu wa wataalamu wa lugha mashuhuri:”Kuna mtu aliniambia kuwa zipo kati ya 20 na 26; mwingine akaniambia zipo 17 zilizoandikwa na...
Malawi: Wanablogu Wajadili Matetemeko ya Ardhi 30 Katika Wiki 3
Katika kile ambacho baadhi ya wataalamu wa miamba wamekieleza kama matukio ya nadra, Wilaya ya Kaskazini ya Karinga nchini Malawi imeshuhudia jumla ya matetemeko ya ardhi 30 katika wiki tatu zilizopita ambayo yamesababisha vifo 5, zaidi ya watu 200 kujeruhiwa na zaidi ya watu 3,000 kupoteza makazi. Wanablogu wamekuwa wepesi kushirikiana maoni.
Malaysia: Mtetezi wa Uhuru wa Vyombo vya Habari Amshtaki Mwanablogu
Mwanahabari-mwanablogu mkongwe anashtakiwa katika kesi ya madai na mwanasiasa anayejulikana kwa kutetea uhuru wa habari nchini Malaysia. Angalia maoni ya wanablogu wa Malaysia.
Rwanda: Video za Wanaojitolea
Mfululizo wa video zilizopakiwa na mtumiaji kdarpa kwenye YouTube, zinaonyesha wafanyakazi wa kujitolea na watu waliokutana nao wakiwa safarini nchini Rwanda ambapo walifanya kazi na jamii za sehemu hiyo.
Ecuador: Serikali Yaifungia Idhaa ya Televisheni ya Teleamazonas
Serikali ya Ecuador iliiondoa idhaa ya televisheni ya teleamazonas kwa masaa 72 kwa kusambaza habari za uongo. Wakosoaji wanaona kuwa hatua hii ni tishio kwa uhuru wa kujieleza.
Iran: Maandamano Tehran
Hii ni video inayoonyesha waandamanaji huko Manzarieh na Nyavaran mjini tehran wakiimba kauli mbiu dhidi ya utawala wa Kiislamu Jumamosi.
China na Iran: #CN4Iran
Jana, maelfu ya Wa-Irani waliingia mitaani ili kupinga dhidi ya utawala wa kiimla. Maandamano hayo yaliwakumbusha watu wa China juu ya vuguvugu la demokrasi la Tiananmen la 1989 na watumiaji wa Ki-China wa twita wanatumia alama ya #cn4iran ili kuonyesha mshikamano na wenzao wa Irani.
Palestina/Gaza: Matayarisho ya Maandamano ya Uhuru Gaza
Ni kama wiki moja hivi mpaka Maandamano ya Uhuru Gaza yatakapoanza. Lengo lake ni kuonyesha mshikamano na Wapalestina na kuongeza ufahamu kuhusu vikwazo vinavyoizingira Gaza. Katharine Ganly anatazama baadhi ya matukio yaliyotokea katika maandalizi ya maandamano hayo.
Singapore: Kampeni ya “Kataa Ubakaji”
Nchini Singapore, mara nyingi kumbaka mke wako hakuchukuliwi kama tendo la kubaka. Waandaji wa kampeni ya “Kataa Ubakaji” wanataka kukomesha sheria inayokinga ubakaji ndani ya ndoa kwa kuzindua kampeni ya kukusanya saini ambazo zitawasilishwa kwa watunga sera. Wengi wa raia wa mtandaoni wanaiunga mkono kampeni hii.