Aprili, 2010

Habari kutoka Aprili, 2010

India, Pakistani: Hekaheka za Sania-Shoaib Zaendelea

  14 Aprili 2010

Utata wa harusi ya Shoaib Malik na Sania Mirza unaendelea huku vyombo vya habari vikichochea hekaheka na mamilioni ya watu nchini India na Pakistani wanaendelea kuzama katika habari hiyo. Wakati wapenzi hao wanajiandaa na harusi na kuvishinda vikwazo, sehemu nyingine mashambulizi yanaendelea.

Piga kura kuchagua “Blogu Bora Zaidi”

  14 Aprili 2010

Upigaji kura mtandaoni umeanza kwa ajili ya Tuzo ya Blogu Bora Zaidi inayotolewa na Deutsche Welle (Shirika la Habari la Ujerumani), moja kati ya mashindano ya blogu yenye hadhi kubwa kimataifa na blogu zilizotajwa kushiriki ni za lugha kumi na moja tofauti. Unaweza kuipigia kura blogu uipendayo hadi April 14, 2010.

Moroko: Je, Wakristu Wako Hatarini?

Mapema mwezi Machi mwaka huu, watazamaji walishuhudia jumla ya wafanyakazi wa muda mrefu katika kituo cha Kikristo cha kulelea watoto yatima wapatao 20 wakifukuzwa kutoka katika nchi ambayo wanaiona kama nyumbani. Tukio hilo pamoja na mengine kadhaa yaliyofuatia yamezusha mjadala kuhusiana na imani ya Kikristu katika ufalme huo.

Urusi: Habari za Mwanzo za Milipuko ya Mabomu

RuNet Echo  9 Aprili 2010

Utaratibu wa Jumatatu asubuhi mjini Moscow ulivunjwa leo na milipuko ya mabomu mawili mabomu ya kujiua, ambayo yaliua watu wapatao 38 na kujeruhi kwa uchache watu wapatao 70. Alexey Sidorenko anatafsiri baadhi ya taarifa za mwanzo kutoka katika ulimwengu blogu za Urusi.

Muziki Wenye Ujumbe – Video Mpya za Muziki Kutoka Tibet

  7 Aprili 2010

Mradi wa kutafsiri Blogu uitwao High Peaks Pure Earth hivi karibuni umetupia jicho “muziki wenye ujumbe” kwa kutafsiri mashairi ya nyimbo za Tibet kutoka video za Muziki zilizowekwa kwenye mtandao. Tarehe 10 Machi mwaka huu , blogu hiyo iliweka video ya hip hop inayoitwa “New Generation” (“Kizazi kipya” kwa Kiswahili)...