Habari Kuu kutoka Julai 2010
Habari kutoka Julai, 2010
Lebanoni: Utawala wa Dinosauri
Punde baada ya matukio ya unyanyasaji ya hivi karibuni nchini Lebanon, Msemo wa “Utawala wa Dinosauri” ulianza kutumika na wanaharakati wa mtandaoni kwenye kampeni dhidi ya uvamizi wa namna hii katika mitandao yao. Mwanablogu wa Lebanon Tony anaeleza maana ya msemo huo.
Palestina: Mateso ya Kuwa Uhamishoni
Wakimbizi wa Kipalestina ni miongoni mwa watu ambao wamejikuta wakikimbilia uhamishoni ulimwenguni kote, Umoja wa Mataifa unatoa msaada kwa jumla ya wakimbizi waliosajiliwa wapatao milioni 4.7 katika ukanda unaokaliwa kwa nguvu huko Palestina, Jordan, Lebanoni na Syria. Mamilioni ya wakimbizi wa Kipalestina na wale walioteguliwa kutoka kwenye makazi yao wanaishi sehemu mbalimbali duniani. However, their Hata hivyo, watu hawa daima mioyo yao ipo nyumbani kwao, au kwa wazazi au mababu na mabibi zao waliobaki nyuma. Wanablogu wawili wa huko Gaza wameandika kuhusu mateso ya kuwa uhamishoni.
Asia ya Kusini Mashariki : Ngono na Udhibiti wa Mtandao
Uratibu wa maudhui katika intaneti unaonekana kana kwamba ni kinyume na demokrasia lakini serikali za Kusini Mashariki mwa Asia zinaweza kuhalalisha kitendo hicho kwa kuzusha haja ya kuwaokoa vijana kutoka kwenye janga la tabia za ngono holela.
Ivory Coast: Mwanablogu na Mwandishi wa Habari Théophile Kouamouo Akamatwa Pamoja na Timu Yake Tangu Julai 13
Waandishi wa habari watatu wa Le Nouveau Courrier d'Abidjan walitiwa mbaroni na polisi baada ya kukataa kueleza vyanzo vya habari vya uandishi wao wa kipelelezi kuhusu biashara ya usafirishaji kahawa na kakao kwenda nje ya nchi. Yafuatayo ni maoni kutoka kwa raia na vyombo vya habari nchini Ivory Coast huku wenzao watatu wakiendelea kupigania kuachiwa kwa wanahabari hao.
Rwanda: Wanaomuunga Mkono wa Paul Kagame Wabaini Nguvu ya Twitter, Facebook na Blogu
Waungaji mkono wa rais Paul Kagame wa Rwanda wameanza kutumia nguvu ya ushawishi ya Facebook, Twitter na blogu ili kumsaidia kushinda uchaguzi wa rais unaotarajiwa kufanyika tarehe 9 Agosti 2010.
Afrika ya Kusini: Dakika 67 za Mabadikio – Siku ya Mandela
Nelson Mandela alitumikia kifungo cha miaka 27 jela kule katika Kisiwa cha Robben, Afrika Kusini. Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kwamba Madiba (kama ambavyo wengi wanapenda kumwita huko Afrika ya Kusini) alitumia miaka 67 ya maisha yake katika kupiga vita ubaguzi wa rangi na umaskini. Jumapili hii Julai 18 2010, kutakuwa na maadhimisho ya miaka yake 92 - na pia Siku ya Mandela - siku ambayo watu duniani kote watajitolea dakika 67 ili kuifanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi kwa wote.
Ghana: Je Una Chumba cha Ziada kwa Ajili ya Rais wa Zamani Rawlings?
Rais wa zamani wa Ghana Jerry Rawlings hana pa kuishi. Anahitaji nyumba ya kupanga katika mji mkuu wa Ghana Accra. yafuatayo ni maoni ya wanablogu wa Ghana pamoja na wasomaji wao.
Cameroon: Vyombo vya Habari Vyachochea Demokrasia
Célestin Lingo anaonyesha uhusiano kati ya vyombo vya habari na mchakato wa demokrasi nchini Cameroon.
China: Kashfa ya Wizi wa Kitaaluma Uliofanywa na Wang Hui, Mtazamo wa Kimataifa
Kuna kashfa ya wizi wa kitaaluma iliyoibuka mwezi Machi katika duru za kitaaluma za Kichina pale Profesa wa Fasihi wa Chuo Kikuu cha Nanjing, Wang Binbin, alipotuhumu kwamba kazi ya uzamizi ya Wang Hui kuhusu Lu Xun – Kugomea Kukata Tamaa – ina aya kadhaa ambavyo vimenukuliwa moja kwa moja...
Uganda: Wanablogu Washtushwa na Milipuko ya Mabomu
Mashabiki wa soka kote ulimwenguni walikusanyika kwenye kumbi za baa na migahawa ili kushuhudia mechi ya fainali za Kombe la Dunia usiku wa Jumapili iliyopita. Nchini uganda usherehekeaji huu ulikatishwa pale milipuko ya mabomu iliposambaratisha maeneo mawili maarufu kwa sherehe za mpaka majogoo jijini Kampala, mji mkuu wa nchi hiyo.