Habari kutoka Novemba, 2013
Mkutano wa Global Voices Cairo, Misri
Mkutano mwingine wa Global Voices unapangwa kufanyika Novemba 16 jijini Cairo, Misri. Tafadhali shiriki na wanachama wetu wa Jumuiya ya GV kwa kusanyiko hili maalumu.
Udadisi wa Sami Anan
Mwanablogu wa Misri Zeinobia anatoa maoni yake machache kuhusu kuibuka tena kwa Sami Anan, Mnadhimu mkuu wa zamani wa Majeshi ya Misri. Je, ana mpango wa kugombea urais? Mwanahabari wa Sauti za Dunia Mtandaoni Victor Salama anasimulia zaidi.
Global Voices Yasaidia Wahanga wa Haiyan Nchini Ufilipino
Kimbunga kijulikanacho kama Haiyan hadi sasa kimeshaua maelfu ya watu nchini Ufilipino. Wiki hii tunaongea na waandishi wetu wlioko nchini Ufilipino pamoja na mfanyakazi anayehusika na misaada kujua ni kwa namna gani tunaweza kutoa msaada wetu.
Misri: “Morsi Hatarudi Madarakani”
Aliyekuwa rais wa Misri Mohamed Morsi hatarudi madarakani, anasema mwanablogu wa Misri Alya Gadi, kwenye mtandao wa Twita. Kuufanya ujumbe wake wazi, ametafsiri kwa lugha mbalimbali: مرسي لن يعود – Morsi is not coming back – Morsi no va a volver – Morsi ne reviendra pas – Morsi kommt nicht zurück...
FIFA Yazipiga Faini Croatia na Ugiriki kwa Tabia ya Mashabiki ya Ubaguzi wa Rangi
Mnamo Novemba 2013, Croatia ilijiunga na orodha ya kuongezeka kwa timu za taifa za kandanda ambazo FIFA imezipiga faini kwa ajili ya tabia za ubaguzi wa rangi ya mashabiki wao au wajumbe wa timu. Mwezi Mei 2013, FIFA ilianza kutekeleza vikwazo vikali dhidi ya ukabila na ubaguzi. Rais wa FIFA...
Serbia Yaibua Maswali Ikiwa Kanisa Lastahili Kusamehewa Kodi
Nchini Serbia ripoti ya uchuguzi uliofanywa na shirika la Serbia la kila siku liitwalo Blic ikiwa Kanisa la Kisabia la Orthodox, ambao viongozi wao hivi karibuni wamekuwa katika vyombo vya habari mara nyingi kutokana na ripoti ya matumizi ya anasa yaonyesha sasa lazima kuanza kulipa kodi. Kanisa la Kisabia la...
Huzuni na Hasira Mjini Kidal, Mali
Mwanablogu Wirriyamu anaomboleza kuuawa kwa waandishi wa habari wawili wa ufaransa [fr] mjini Kidal, Mali. Lakini kando na huzuni yake kubwa, Wirriyamu pia anajisikia hasira kwa kuona kaskazini mwa Mali inaendelea kutaabika tena kwa mashambulizi ya kigaidi. Anaandika kuhusu hasira ya kimya chake kuhusu hali ya mambo: Tant qu’il ne...
Iran: Hukumu ya Jela ya Mwanablogu Yapunguzwa Hadi Miaka 17
“Haki kwa Hossein Derakhshan” blogu ilitangaza mnamo Oktoba 16, 2013 kwamba mamlaka ya Iran imepunguza kifungo cha jela cha mwanablogu wa Iran Hossein Derakhshan (pia anajulikana kama “Hoder”) hadi miaka 17 kutoka miaka 19.5 Derakhshan alikamatwa mnamo Novemba 1, 2008.
Wa-Malawi Wajiandae kwa Kashfa Zaidi za Ufisadi
Steve Sharra anaelezea kwa nini Wamalawi wanakabiliwa na kashfa ya zaidi za ufisadi baada habari kuwa wazi kwamba baadhi ya wa-Malawi wenye nguvu walitumia vibaya Mfumo wa Pamoja wa Ndani wa Udhibiti wa Fedha kupora mabilioni ya fedha za umma: Kutokuwepo kwa usawa wa kijamii kunajenga ufa mkubwa miongoni mwa...
Filamu 14 za Mazingira zenye Kuvutia
TVE (Televisheni inayohusika na Mazingira) yaonesha video 14 bora za washindani waliofika fainali kwenye shindano la kimataifa la filamu bora ya mazingira. Washiriki kutoka sehemu mbalimbali za dunia wametengeneza filamu zinazochukua muda wa dakika 1 kwa kuzingatia mada zinazohusiana na mabadiliko ya hali ya hewa, maendeleo endelevu pamoja na bayoanuai....