Habari kutoka Novemba, 2009
Amerika ya Kati: Kasi Kubwa ya Ueneaji wa Jangwa
Ueneaji wa jangwa unasambaa kimyakimya lakini kwa kasi kubwa mahali pengi duniani na Amerika ya Kati haijaweza kukwepa hali hii iliyo na athari mbaya za kutisha. Wakati ambapo majangwa ni maumbo ya asili, ueneaji wa jangwa ni mchakato wa kuharibika kwa nyanda za ardhi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na uharibifu unaofanywa na binadamu.
Kutambulisha Sauti Zinazotishwa
Leo, kitengo cha utetezi cha Global Voices, kinazindua tovuti mpya inayoitwa Threatened Voices, yaani, Sauti Zinazotishwa ili kusaidia kufuatilia unyamazishaji wa uhuru wa kujieleza wa mtandaoni. Inaonyesha ramani ya dunia na mwingiliano wa saa unaosaidia kuonyesha taarifa za vitisho na ukamataji unaofanywa dhidi ya wanablogu duniani kote, na ni mhimili mkuu wa kukusanyia taarifa kutoka katika asasi na wanaharakati walioamua kujitoa muhanga kwelikweli.
Tamasha la Blogu Indonesia
Tulitembelea tamasha la blogu la Indonesia au PestaBlogger 2009. Hii nim ara ya tatu kwa tukio hili la mwaka kufanyika. Tukio hili lilishuhudia wanablogu kutoka kila sehemu ya Kisiwa hiki ambacho pia ni Taifa wakimiminika mjini Jakarta ili kusherehekea, kujadili na kujumuika.
Misri: Mwanablogu wa Kiume Aagizia Bikra ya Bandia
Mengi yalisemwa na kuandikwa juu ya zana ya kutengeneza bikra ya bandia - mpaka mwanablogu Mmisri wa kiume Mohamed Al Rahhal akanunua moja. Marwa Rakha anatuletea habari hiyo.
Vietnam: Matangazo Mengi Katika Uwanja wa Ndege
Charvey amebaini matangazo mengi kuliko kawaida katika uwanja wa ndege wa Vietnam.
Afrika: Chungu cha Kuiyeyusha Afrika
Marvin anaandika kuhusu Afripot, tovuti ya habari inayotilia makini habari za Afrika: “Hivi sasa anatambulisha chungu cha kuyeyushia Afrika – Afripot. Tayari nimo ndani ninayeyuka na ninatumaini kukuona pale na wewe pia kwani mazungumzo kuhusu Afrika na Waafrika yanachukua kasi na kupamba moto. Ni nani ajuaye, inaweza kutengeneza joto la...
Ujauzito na Magereza: Afya na Haki za Wanawake Magerezani
Mapambano bado yanaendelea kuhakikisha haki za binadamu kwa wanawake wajawazito duniani pote, ni inaelekea kwamba katika mchakato huo, wanawake waliopo magerezani wanasahauliwa. Je ni hatua zipi zilizochukuliwa kuhakikisha kuwa nao wanaangaliwa kwa utu, kwa kuzingatia uhai wanaoubeba.
Georgia: Aibu Katika Kanisa la Orthodox
Katika nchi inayofuata dini zaidi kwenye maeneo ya kusini mwa Caucasus ambako mkuu wa Kanisa la Orthodox (madhehebu ya Kanisa la zamani au kihafidhina) anaweza kuhamasisha ongezeko la watoto, kukosoa watumishi wa kanisa bado ni mwiko. Kuwatania, hata hivyo, ni jambo baya zaidi na lililojaa hatari.
Kenya: Ramani Mpya Ya Wazi ya Kitongoji Cha Kibera Kwenye Blogu
Mradi wenye lengo la kutengeneza ramani mpya ya wazi ya kitongoji cha Kibera mjini Nairobi, Kenya: “Na jana tulimaliza siku nzima pale MS Action Aid kenya, ambako wanafunzi wa ki-Denmark pamoja na wengine waliotokea kwenye mashirika mbalimbali kama vile Ushahidi, UNICEF, Umande Trust na World Bike, walipoonyeshwa mbinu za kutengeneza...
Iran: Majeshi Ya Usalama Yawashambulia Waandamanaji
Kwa mujibu wa Kian majeshi ya usalama yaliwashambulia waandamanaji katika viwanja vya hafteh tir mjini Teheran na kuwajeruhi watu kadhaa.