Habari kutoka Novemba, 2009
Ofisa Aweka Wazi Ufisadi wa Polisi kupitia Mtandao
Mnamo tarehe 6 Novemba, afisa wa polisi katika Idara ya Mambo ya Ndani huko Novorossiysk alitumia tovuti yake binafsi kuwasiliana na Waziri Mkuu Vladimir Putin na kuzungumzia matatizo lukuki yanayowakabili maafisa wa polisi nchini Urusi.
Kenya: Mwai Kibaki na Odinga Budi Washirikiane na ICC
Ubia wa Kuleta Mabadiliko umetoa tamko linalowataka mwai kibaki na raila odinga kushirikiana na mahakama ya kimataifa ya Jinai na kuhakikisha muswada wa Tume Maalum unapitishwa nchini kenya na kurasimishwa kama sheria ndani ya wiki mbili.
Vijana wa Kiyahudi na Kipalestina Watumia Video Kuuelewa Mgogoro
Mashirika mawili tofauti nchini Israel na katika Majimbo ya Palestina yanatumia zana za video ili kuwasaidia vijana wa Kiarabu na Kiyahudi kuuelewa mgogoro na kujenga daraja kati yao.
Nepal: Mapinduzi Ya Gesi Inayotokana na Samadi
Nchini Nepal karibu asilimia 87 ya kaya zinategemea kuni kama chanzo cha nishati. Hata hivyo, vituo vya kuzalisha gesi inayotokana na samadi vinajitokeza kwa idadi kubwa nchini Nepal na kuanzisha mapinduzi ya kijani.
Cuba: Ukweli wa Sanchez Kutiwa Mbaroni Waibuka
Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika vyombo vikubwa vya habari na katika ulimwwengu wa blogu pamoja na ule wa Twita. Yoani ameandika (es) kuhusu tukio hilo...
Yoani Sanchez Pamoja na Wanablogu Wengine wa Cuba Wakamatwa na Kupigwa
Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú iliweka kiungo kuelekea makala iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na mchangiaji wa Global Voices Claudia Cadelo, walitiwa mbaroni na majeshi ya usalama. Habari mpya kutoka kwa Penultimos Días zinataarifu kuwa...
Bolivia: Uhaba wa Maji Kwa Sababu ya Theluji Inayoyeyuka
Safu ya milima ya Chacaltaya ina baadhi ya vilele ambavyo ni alama zenye maana katika safu ya milima Andes iliyopo Bolivia. Kwa kuwa ilikuwa ni sehemu moja pekee ambapo mchezo wa kuteleza barafuni uliweza kufanyika katika nchi hii ya milimamilima, milima hii ni maarufu sana kwa wale walio kwenye Idara...
Ghana: Vionjo Sehemu ya Kwanza
Sehemu ya kwanza ya vionjo vya Ghana iliyotayarishwa na Gayle: Nchini Ghana, kila kanda ina kitu cha kutoa. Utamaduni, historia, pwani, wanyama na mimea, unaweza ukavivinjari nchini kote, kutokea kwenye mitisitu ya kitropiki kule kusini mpaka mbuga za savana za kaskazini. kama ni mpenzi wa pwani au historia, utaburudika na...
Tunisia: Mwanablogu Fatma Arabicca Awekwa Kizuizini
Mwanablogu wa Kitunisia Fatma Riahi ambaye hublogu kama Fatma Arabicca, ameshtakiwa kwa udhalilishaji katika blogu yake na hivi sasa amewekwa kizuizini.Kundi limeundwa kwenye Facebook kumuunga mkono mwanablogu huyu mwenye umri wa miaka 34, ambaye pia anatuhumiwa kublogu kwenye Debat Tunise (Mdahalo wa Tunisia).
Irani: Vuguvugu la Kijani Laupinga Utawala Tena
Upande wa upinzani wa Vuguvugu la Kijani nchini Irani mnamo tarehe 4 Novemba uliendesha maandamano makubwa ambapo maandamano hayo yalikabiliwa na matumizi makubwa ya nguvu ya kuyazuia yaliyofanywa na vikosi vya usalma. Kama ambavyo sasa inatarajiwa, uandishi wa habari wa kiraia nchini Irani haukukosa kitu kwani ulirekodi 'historia' hiyo kupitia simu zao za mikononi.