Habari kutoka Novemba, 2009
Jordan: Barua kwa MBC
M-jordan Ola Eliwat, kutoka Cinnamon Zone, anaandika barua ya wazi kwa makapuni ya televisheni ya MBC. Katika barua hiyo anaandika: “Na tafadhali fikirieni kufunga 90% ya idhaa zenu, nadhani itakuwa hisani KUBWA kwa taifa la Kiarabu!”
Philippines: Mti wa Dita Waokoa Maisha ya Watu 36 Wakati wa Mafuriko
Mti wa aina ya Dita huko Manila mjini uligeuka kuwa "Mti wa Uzima" wakati ulipotumika kama kimbilio na wakazi ambao walitegwa kwenye nyumba zao wakati wa janga la kimbunga na mafuriko ya hivi karibuni. Somo: Usikate miti.
Uganda: Ugonjwa wa Panzi Waota Mizizi
Wanasiasa wa Uganda wanakuwa kama panzi: “kufuatia hali ya kufikia kikomo kwa tawala nyingi za kiimla, Museveni na washirika wake katika ukaliaji wa mabavu wa Buganda kwa kutumia silaha wanaanza kuwa kama panzi.”
Venezuela: Kukutana na kazi za msanii Jesus Soto
Kazi za msanii wa Kivenezuela Marehemu Jesus Soto zinapaswa kuguswa na kujizamisha ndani yake ili kuzielewa. Wachache waliwahi kutembelea kazi zake kwenye makumbusho wameandika uzoefu wao.
Cameroon: Wezi “wakarimu” na Malipo kwa Kutumia Salio la Simu
Karibu wakazi milioni 20 wa Cameroon wanakabiliwa na kiwango kinachoongezeka cha unyang’anyi. Majambazi wameweza hata kuyavamia makao makuu ya taifa ya polisi na Wizara ya Mambo ya Nje katika mji mkuu wa Yaounde.
Video: Dunia Yaadhimisha Kuanguka kwa Ukuta wa Berlini
Leo ni Kumbukumbu ya 20 ya kuanguka kwa Ukuta wa Berlini, kizingiti madhubuti cha kiusalama ambacho kiliwahi kuligawa jiji la Berlini katika pande mbili za Mashariki na Magharibi huko Ujerumani. Leo tunaonyesha baadhi ya picha za video zinazotoka pande mbalimbali za dunia zinazopandishwa ili kusherehekea siku hii na nini ukuta huo ulimaanisha siyo Ujerumani tu bali duniani kote.
Afrika Kusini: Wimbo wa Taifa kwa Wanaoongea Kiingereza
Wimbo wa Taifa wa Afrika Kusini kwa wanaoongea Kiingereza: Ni njia kuu iliyoje ya kufafanua kwa kuonyesha Wimbo wa taifa wa Afrika Kusini kwa wale kati yetu ambao kwanza hatuufahamu mpaka sasa, pili tunaoufahamu lakini pengine hatujui jinsi ya kutamka maneno yake na tatu ambao hatuongei lugha iliyo kwenye wimbo...
Naijeria: Wanablogu Wajadili Sifa Mbaya ya Naijeria
Inajulikana vyema kuwa Naijeria ina tatizo la muonekano – utapeli wa 419 kwenye intaneti, rushwa, uharamia wa mafuta katika jimbo la Delata – kwa watu wengi, huu ndio uhusiano unaokuja akilini wakati nchi yenye watu wengi zaidi Afrika inapotajwa.
Angola: Gharama za Juu za Maisha Mjini Luanda
Gharama kubwa ya maisha nchini haieleweki: viashiria vya maendeleo vya hali ya juu havishabihiani na hali ya kifedha ya Waangola wengi na havitafsiriki katika viwango vya maisha vya wasio na hali nzuri kiuchumi.
Naijeria: Ken Saro-Wiwa Akumbukwa
Chidi Opara anamkumbuka Ken Saro-Wiwa, Mwandishi wa Kinaijeria, mwanaharakati wa mazingira na haki za walio wachache ambaye aliuwawa na watawala wa kijeshi wa Naijeria tarehe 10 Novemba, 1995.