Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Februari, 2010
Chile: Tetemeko Kubwa la Ardhi lenye Ukubwa wa 8.8 Laikumba Chile
Saa 9:34 usiku kwa saa za Chile, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.8 liliukumba mwambao wa eneo la Maule nchini Chile. Tetemeko hilo liliutetemesha mji mkuu wa Santiago uliopo Kilomita 325 kutoka katika kiini cha tetemeko hilo. Uharibifu mkubwa umeripotiwa nchin nzima, na idadi ya waliofariki inazidi kwenda juu.
Nijeria: Baada ya miezi miwili bila uongozi, kaimu Rais mpya
Baada ya wiki za mivutano ya kisiasa, Baraza la Seneti lilimthibitisha Goodluck Jonathan kama kaimu Rais. Wengi kwenye ulimwengu wa blogu waliliona tukio hilo kama sababu ya kusherehekea… lakini wengine waliliona kama jambo la kutia hofu, wakieleza kwamba japokuwa kutwaa madaraka kwa Jonathan kunaweza kuwa ni ulazima wa kisiasa, kutwaa huko hakujaruhusiwa wazi na katiba ya Naijeria.
Ethiopia: Wanablogu walitetea Shirika la Ndege la Ethiopia baada ya ajali ya ndege
Wanablogu waishio Ethiopia wameharakia kuitetea rekodi ya usalama wa safari za ndege za nchi hiyo siku ya Jumatatu baada ya ndege moja kuanguka karibu na Beirut, ikihofiwa kupoteza maisha ya watu wote 90 waliokuwepo.
Misri: Mwanablogu apoteza kazi kwa kufichua ukweli kuhusu habari ya bikra za bandia
Mwanablogu ambaye pia ni mwanahabari wa Kimisri Amira Al Tahawi amefukuzwa kazi kwa kufichua ukweli kuhusu habari ya uongo juu ya bikra za bandia zinazotengenezwa China katika makala alioyoichapa kwenye yake, ndivyo wanavyodai wanablogu. Yafuatayo ni baadhi ya maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu za Kimisri kuhusu kisa hicho.
Haiti: Kwa Nini Habari Zote Hizi Kuhusu Yatima?
Mwezi mmoja baada ya tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa poiti saba kuangamiza sehemu kubwa ya Haiti ya kusini, mustakabali wa watoto, na hasa hasa yatima, umekuwa ni habari kubwa katika kona mbalimbali. Lakini sauti za Wahaiti kwenye mada husika zimekuwa chache...
Mapinduzi Nchini Niger: Wanablogu Wapumua Pumzi ya Ahueni
Alhamisi Februari 18 mapinduzi ya kijeshi yalifanyika nchini Niger ambayo kwayo Rais Mamadou Tandja alikamatwa baada ya mapambano ya bunduki katika mji mkuu, Niamey. Miezi michache iliyopita Tandja alibadilisha katiba kinyume cha sheria ili ajiruhusu kuongoza kwa muhula wa tatu katika kile ambacho kilionekana kama dhuluma ya halaiki kwenye kura maoni. Wanablogu wanatoa mitazamo yao juu ya maendeleo haya mapya.
Upinzani Waongezeka dhidi ya Mapendekezo ya Tanzania na Zambia katika Makubaliano ya CITES
Upinzani unaongezeka dhidi ya mapendekezo ya Zambia na Tanzania ya kuruhusiwa na Makubaliano ya Biashara ya Kimataifa ya Makundi ya Mimea na Wanyama Walio Katika Hatari ya Kutoweka (CITES), kuuza hifadhi ya pembe za ndovu walizonazo.
India: Ugaidi Waikumba Pune
Mnamo majira ya saa 1:30 jioni (Februari 13, 2010) mlipuko wa bomuuliua watu 9 na kuwajeruhi wengine 57 katika mgahawa maarufu kwa watalii uliopo katika mji wa Magharibi wa Pune, India. Hisia ziko juu huku wanablogu na watumiaji wa twita wakitoa maoni.
Malaysia: Harakati za Kutovaa Nguo za Ndani Wakati Wa Siku ya Valentino
Wanafunzi kadhaa wa kike nchini Malaysia wanahamasisha "harakati za kutovaa nguo za ndani" katika siku ya Valentino. Kampeni hiyo imepata umaarufu mno kupitia ujumbe wa mtu kwa mtu na kwa kupitia intaneti. mamlaka za kidini hazijafurahishwa. Wanablogu wanatoa maoni.
Tangazo la Mkutano Mkuu wa Uanahabari wa Kiraia wa Global Voices 2010
Tunayo furaha kutangaza Mkutano Mkuu wa Uanahabari wa Kiraia wa Global Voices 2010! Mwaka huu mkutano wetu utafanyika katika mji mchangamfu wa Santiago, Chile tarehe 6-7, 2010.Kati ya vivutio vya mkutano huo kitakuwa ni kutangazwa kwa washindi wa Tuzo Ya Kuvunja Mipaka, tuzo mpya iliyoundwa na Google pamoja na Global Voices.