Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Agosti, 2010
Tunisia: Picha ‘Zilizochakachuliwa’ ni Dalili ya Hali Halisi katika Vyombo vya Habari vya Kitaifa
Utumiaji vyombo vya habari vya kitaifa nchini Tunisia kama chombo vya kupigia propaganda ni jambo ambalo limeripotiwa vya kutosha. Ushahidi wa hivi karibuni kabisa wa utumiaji mbaya wa vyombo vya habari umewekwa bayana na wanablogu wa nchi hiyo mnamo tarehe 20 Agosti baada ya magazeti ya Le Temps na Assabah kuchapisha ripoti kuhusu taasisi ya hisani ya Zeitouna kutuma msaada wa kibinadamu wa chakula kwa waathirika wa mafuriko nchini Pakistani.
Irani: Kampeni ya Kutaka Mwanablogu-Mpiga Picha Hamed Saber Kuachiwa Huru
Zaidi ya wanafunzi 70 waliohitimu elimu ya chuo kikuu na wasomi wa nchini Irani wametoa wito wa kuachiwa kwa Hamed Saber, ambaye ni mwanablogu-mpiga picha na mwanasayansi wa kompyuta wa nchini humo aliyekamatwa pasipo sababu za kuelewekea mnamo tarehe 21 Juni 2010 jijini Tehran.
Mashindano ya Video: Intaneti Kama Chombo cha Kueneza Amani
Mfumo wa Intaneti umependekezwa kwa ajili ya kupata Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mwaka 2010. Kama sehemu ya mjadala unaoendelea kuhusu mchango wa Intaneti katika jamii nzima ya binadamu , Condé Nast na Google Ireland wameungana na kuandaa mashindano haya ya video na mshindi atapata fursa ya kusafiri na pia video yao kuoneshwa kupitia MTV ya Italia.
Ufilipino: Maoni ya Wanablog Juu ya Elimu ya Ya afya ya Uzazi
Mwaka huu wa masomo serikali ya Philippines inatekeleza mpango wa elimu ya uzazi kwenye shule za umma unaofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya watoto na vijana. Na wanablogu wametoa maoni juu ya suala hilo.
Korea Kusini: Maombolezo ya Kitaifa ya Mwanamwali wa Kivietnam
Mwanamwali mdogo wa Kivietnam aliuwawa na mumewe wa Kikorea nchini Korea. Wanablogu wa Korea wanatoa rambirambi zao kwa kifo kibaya cha mke huyo mwenye umri mdogo huku wakiitaka serikali kutokomeza eneo hili lisiloonekana kwa urahisi la haki za binaadamu, linalohusiana na wachumba kutoka nchi za kigeni.
Italia: HAPANA kwa Vikwazo Dhidi ya Uhuru wa Kujieleza wa Mtandaoni
Muswada mpya wa habari na Unasaji wa siri wa Mawasiliano ambao umewasilishwa kwenye bunge la Italia unaweza kuanzisha "hatari ya malipo ya fidia" kwa wanablogu wote na vyombo vya habari vya mtandaoni.
Udhibiti Nchini Singapore
Singapore imesababisha kelele kubwa baada ya kupiga marufuku filamu ya aliyewahi kuwa mfungwa wa kisiasa na kumkamata mtunzi Mwingereza wa kitabu kilichoandiaka kuhusu adhabu ya kifo nchini humo. Wanablogu wanajadili.