Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Mei, 2014
Polisi wa Masedonia Wawalazimisha Waandishi Kufuta Picha za Ghasia
Ghasia, zilizofumuka baada ya kuuawa kwa kijana wa miaka 19, zilisababisha misuguano kati ya watu wenye asili ya Albania na Masedonia kwenye jiji la Skopje.
Rwanda: Mema, Mabaya na Matumaini
Ingawa Rwanda imepiga hatua kubwa katika kuponya majeraha ya mauaji ya kimbari ya 1994, makundi ya utetezi yanaripoti vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu.
PICHA: Watu 20,000 Waandaman huko Macau China Kupinga “Muswada wa Ulafi”
Muswada utampa mkuu wa serikali jimboni Macau, nchini China, kinga ya kushitakiwa kwa makosa ya kijinai wakati akiwa madarakani na ataaendelea kupata mshahara wake hata baada ya kuondoka madarakani.
Baada ya Miezi Sita, Waathirika wa Kimbunga Haiyan Waendelea Kudai Msaada na Haki
Miezi sita baada ya kimbunga kikubwa kuharibu mamiliaoni ya makazi katika eneo la katikati ya Ufilipino, wahanga wanaendelea kuomba misaada na kutendelewa haki. Kuna madai ya kukosekana kwa mpango wa kurejesha hali kuwa ya kawaida.
Mazungumzo ya GV: Kupigania Kuachiliwa Huru kwa Wanablogu wa Ethiopia wa Zone 9
Wanablogu tisa ikiwa ni pamoja na waandishi wa habari ---wanne wao wakiwa ni wanachama wa Global Voices ---wanashikiliwa nchini Ethiopia kwa sababu ya kutekeleza majukumu yao. Fahamu namna ya kuunga mkono kampeni ya #FreeZone9Bloggers!
Mzee wa Kimasedonia Apambana Kurejeshewa Mali Yake
Mwanablogu wa Kimasedonia anayeitwa Dushko Brankovikj, ambaye mali zake zimetaifishwa mara mbili, ameshinda kesi, lakini serikali haijaweza kumrudishia mali zake.
PICHA: Waandamanaji Nchini Taiwani Wageuza Uzio wa Polisi kuwa Mapambo
Polisi waliweka uzio wa kuwapa tahadhari waandamanaji kuzunguka majengo ya serikali katika jitihada za kuwazuia waandamanaji kukusanyika. Wataiwani wakawajibu kwa kile kinachoonekana kuyageuza mabango hayo ya tahadhari kuwa mapambo.
Mazungumzo ya GV: Je, Utamaduni Ulisababisha Washindwe Kuokolewa Kwenye Ajali ya Kivuko?
Mitazamo potofu kuhusu Wakorea Kusini inaendelea kusambaa kwenye habari zinazotangazwa kuhusu kivuko kilichozama. Je, wahanga hao walikuwa na utii uliopindukia kiasi cha kushindwa kuokolewa?