Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Juni, 2012
Misri: Yatambulisha Kipimio cha Morsi
Baada ya miaka 32 ya Hosni Mubarak, Misri imepata rais mpya Mohamed Morsi, na pia kitumizi cha kufuatilia utendaji pamoja na maendeleo ya kutimiza ahadi kuu 64 alizozitoa rais huyo mteule wakati wa kampeni za uchaguzi nchini humo.
Mabadiliko ya Mfumo wa Ustawi wa Jamii ya Kiafrika
Utekelezaji wa mifumo ya hifadhi ya jamii ya taifa bado uko katika hatua za mabadiliko katika nchi nyingi za Afrika. Mafanikio ya mifumo iliyopo yanajadiliwa na wataalamu wa hifadhi za jamii katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara.
Korea ya Kusini: Mabadiliko ya Sheria kuhusu Uzazi wa Mpango Yaibua Mjadala Mkali
Mamlaka ya Chakula na Dawa ya nchini Korea imetangaza kwamba dawa za kuzuia mimba za dharura zinazofahamika kama 'morning-after pills' zitaanza kupatikana kwa wingi. Hata hivyo, dawa za kuzuia mimba zisizo za dharura zimekuwa dawa za kuandikwa na daktari. Mabadiliko haya ya ghafla kuhusu dawa za kuzuia kuzaliana limeibua mjadala mkubwa mtandaoni.
Zambia Yapanga Bei ya Mahindi kwa Mara Nyingine, Yaikasirisha Benki ya Dunia
Kupanda kwa bei ya mahindi, chakula kikuu nchini Zambia kumesababisha raia kufanya ghasia na hata kusababisha jeshi kuingilia kati. Pamoja na tahadhari iliyotolewa na benki ya dunia kwamba hatua hiyo ingeathiri sekta ya kilimo, watawala wa nchi hiyo wameendelea kupanga bei ya unga wa mahindi.
Kenya: Habari za Mlipuko Jijini Nairobi Zatawala Mijadala ya Twita
Kufuatia mlipuko mkubwa ulioathiri vibaya mtaa mkubwa wa Nairobi, Moi Avenue, wakenya na marafiki wa Kenya walitumia mtandao wa twita kuhabarishana, na kusambaza taarifa, kushauriana na kujadili tukio hilo baya.
Lesotho: Uchaguzi wa amani ambao hukuusikia
Lesotho, nchi ndogo inayozungukwa na Afrika Kusini pande zote, ilifanya uchaguzi wa wabunge Jumapili, uchaguzi ulioendeshwa kwa utulivu, lakini uchaguzi huo haukupewa uzito na vyombo vikuu vya habari.