· Aprili, 2013

Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Aprili, 2013

Urusi: Wapinzani Wapumbazwa na Uchaguzi wa Awali, Wapoteza Uchaguzi Halisi

RuNet Echo  30 Aprili 2013

Mwezi Agosti (mwaka 2012), Mtandao wa Sauti za Dunia uliripoti habari za wanaharakati kadhaa wanaohusika na vuguvugu la maandamano nchini Urusi wanaogombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa. Walitumaini itakuwa rahisi kushinda uchaguzi huo mdogo, ambao ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita. Oktoba 14, 2012 huku idadi ya ndogo ya wapiga kura wakiojitokeza tena ndani ya madai ya siku nyingi ya wizi wa kura katika uchaguzi, Warusi walishiriki kwa maelfu katika uchaguzi nchini kote, kupiga kura kuwachagua mameya wa miji, madiwani, na wabunge wa mikoa.

Irani: Je, Dola Inamwogopa Msichana wa Miaka 13?

Kuwapiga watu marufuku kusafiri nje ya nchi yamekuwa mazoea ya serikali ya Irani  kwa makusudi ya kuwaghasi wanaharakati wa asasi za kisiasa na zile za kiraia kwa miaka mingi. Lakini, mahakama ya usalama iliwasha moto upya kwa kumpiga marufuku kusafiri nje ya nchi mume wa mwanasheria wa haki za binadamu aliyefungwa Nasrin Sotoudeh pamoja na binti yao mwenye umri wa miaka kumi na mitatu, Mehraveh Khandan. Nasrin Stoudeh amehukumiwa miaka kumi na moja gerezani.

Bangladesh: Jengo Laporomoka, Mamia Wauawa kwenye Vifusi

  29 Aprili 2013

Janga jingine tena la kiwanda nchini Bangladesh, safari hii jengo la ghorofa tisa lilianguka na kuua zaidi ya watu 142 na watu wengine karibu elfu moja kujeruhiwa. Watu wengine wengi bado wamenaswa kwenye kifusi na harakati za kuwaokoa bado zinaendelea. tukio hili linatokana na uzembe wa baadhi ya watu kwani utawala wa kiwanda hiki uliwashinikiza watu kuendelea kufanya kazi katika jengo ambalo halikuwa salama.

Serikali ya Bangladeshi Yawafuatilia Wanablogu, Yawatuhumu Kuukashfu Uislam.

  28 Aprili 2013

Kadri mapambano makali kati ya wanaharakati wa Kiislamu na serikali yanavyoendelea kusababisha migongano ya kidini nchini Bangladesh, Mamlaka ya Mawasiliano ya nchi hiyo imechukua hatua ya kuwanyamazisha wanablogu wanaoonekana wapinzani wa Uislamu na serikali. Asif mshindi wa tuzo ya mwanablogu bora amekuwa akilengwa na hatua hizo kwa siku za hivi karibuni.

Iran: Wakati Matetemeko yanaua, “Televisheni Zinafundisha Sala”

Matetemeko makubwa mawili ya ardhi yalilitikisa eneo la kaskazini magharibi nchini Iran, Mashariki jimbo la Azarbaijan mnamo Jumamosi (Agosti 11, 2012), na kuua watu 250 na kujeruhi karibu 1800. Matetemeko ya ardhi kipimo cha 6.4 na 6.3 katika ukubwa, na kusababisha uharibifu mkubwa na mateso. Wa-Irani waliingia kwenye mtandao wa intaneti ili kuwaombolezea wahanga na kuomba watu kujitolea damu na msaada. Pia walionyesha hasira zao kwa televisheni ya kitaifa ya Iran, ambayo hutangaza vipindi vya dini, badala ya kutoa taarifa kwa watazamaji kuhusu matetemeko ya ardhi na jinsi ya kusaidia.

Misri: Mubarak ahukumiwa kifungo cha maisha

Dunia ilishuhudia wakati mahakama ya Misri  ilipomhukumu aliyekuwa Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak na Waziri wake wa Mambo ya Ndani Habib Al Adly kifungo cha maisha hivi leo kufuatia kukutwa na hatia ya kuhusika na mauaji ya waandamanaji.  Hukumu hiyo ilifikiwa baada ya vikao 49,  masaa 250, na kuandikwa katika kurasa 60,000.

Syria: Kutwiti Kutokea Vitani Jijini Aleppo

Mwandishi wa Habari Jenan Moussa amerudi mjini Aleppo, nchini Syria, akitwiti tajiriba yake wakati vita kati ya vikosi vinavyopinga serikali na vile vinavyoiunga mkono serikali inavyozidi kushika kasi. Twiti za Moussa ni za kawaida na za kibinafsi sana, zikiwapa wasomaji wake taswira ya maisha yalivyo kwa wale walio kwenye uwanja wa vita.