Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Januari, 2011
Sudani: Kura ya Maoni ya Sudani ya Kusini katika Picha
Kura ya maoni inaendelea kupigwa huko Kusini mwa Sudani tangu tarehe 9 mpaka 15 Januari 2011 kuamua iwapo sehemu hiyo ya kusini itaendelea kubaki kuwa sehemu ya Sudani ama iwe nchi huru inayojitegemea. Hizi ni picha zinazoweka kumbukumbu muhimu ya kihistoria ya kura hiyo ya maoni katika Sudani ya Kusini.
Sudan: Muda mfupi Kuelekea Kwenye Kura ya Maamuzi ya Sudani ya Kusini
Sudani ya Kusini itaendesha kura ya maoni ili kuamua ikiwa iendelee kubaki kuwa sehemu ya Sudani ama la ifikapo tarehe 9 Januari 2011. Kuna uwezekano ni mkubwa kuwa nchi hiyo kubwa zaidi katika bara la Afrika itagawanyika kuwa nchi mbili zinazojitegemea. Hapa ni maoni ya hivi karibuni zaidi kwenye makala za blogu kuhusu kura hiyo ya maoni. Southern Sudan will hold a referendum on whether or not it should remain as a part of Sudan on 9 January 2011. It is most likely that Africa's largest country will split into two. Here's our latest roundup of blog posts about the referendum. Southern Sudan will hold a referendum on whether or not it should remain as a part of Sudan on 9 January 2011. It is most likely that Africa's largest country will split into two. Here's our latest roundup of blog posts about the referendum.
Tunisia: Anonymous Dhidi ya Ammar – Nani Atashinda Vita ya Kuchuja Habari?
Kichuja habari cha Tunisia, kinachojulikana kama Ammar, kinaeendelea kutishia kuziharibu na kuzifunga anuani za wanaharakati wa mtandaoni, katika nchi hiyo ambayo imekuwa ikishuhudia wimbi la maandamano tangu katikati ya mwezi Desemba. Ni leo tu, wanaharakati wamedai kwamba serikali imeingilia anuani zao za barua pepe,na kuziingilia blogu na mitandao yao ya kijamii, na kuzizuia zisifanye kazi. Hatua hii inaonekana kuja kama kulipiza kisasi kwa shambulio lililofanywa na kikundi cha wanaharakati wa mtanda0ni wanaojulikana kama Anonymous, ambalo lililenga njia na mitandao ya muhimu ya Serikali ya Tunisia.